Savvy FM

Jamii yaonya unyanyapaa dhidi ya warahibu wa dawa za kulevya

2 Aprili 2026, 13:50

Afisa kutoka mamlaka ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevvya kanda ya kaskazini Brenda Mbati akizungumza katika studio za Savvy FM. Picha na Mariam Mallya

Jamii imeaswa kuacha kuwanyanyapa warahibu wa dawa za kulevya kwani kufanya hivyo hupelekea waathirika hao kushindwa kufikia huduma za matibabu.

Na Mariam Mallya

Afisa Kutoka mamlaka ya kudhibiti na kupambana na Dawa za kulevvya kanda ya kaskazini Brenda Mbati amesema familia zinapaswa kuwapokea na kuwasaidia warahibu kwa kuwatafutia matibabu badala ya kuwatenga.

Akizungumza na Savvy FM afisa huyo amesema Urahibu ni ugonjwa kama magonjwa mengine hivyo jamii haipaswi kutumia lugha za kuwanyanyapa kama kuwaita majina yasiofaa kama vile teja, chizi na mengineyo.

Afisa Kutoka mamlaka ya kudhibiti na kupambana na Dawa za kulevvya kanda ya kaskazini Brenda Mbati

Arafa Ally ni miongoni mwa aliyewahi kuwa mrahibu wa dawa za kulevya amesema urahibu ulimuathiri kwa kiasi kikubwa na kupelea kupoteza familia yake .

Sauti ya Arafa Ally aliyewahi kuwa mrahibu wa dawa za kulevya