Savvy FM

Soko la kisasa Arusha tumaini jipya kwa wafanyabiashara

June 18, 2025, 5:25 pm

Mkuu wa mkoa wa Arusha Paul Makonda akizungumza wakati wa utiaji saini ujenzi soko la kisasa la Machinga.Picha na Mariam Mallya.

“Mipango ya ujenzi na miradi inayoendelea hii Makonda hakujanayo ni miradi ilikuwepo ili soko lilipaswa kujengwa na pesa ilitolewa toka 2021 shilingi millioni 500 pesa zimekaa kwenye akaunti”.

Na Mariam Mallya

Mkuu wa mkoa wa Arusha Paul Makonda ameongoza mamia ya wananchi wa jiji la Arusha kushuhudia hafla ya utiaji saini ujenzi wa Soko la Machinga (Machinga Business Park) eneo la Morombo na uwanja wa mpira wa Arusha City Club katika kata ya Murieti, Jiji la Arusha.

RC Paul Makonda ameishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kutekeleza ilani ya chama cha Mapinduzi kwa kuendelea kutenga fedha kwa ajili ya miradi ya maendeleo mkoani Arusha.

Sauti ya Mkuu wa mkoa wa Arusha, Paul Makonda

Akiwasilisha taarifa za mradi wa uwanja wa mpira wa Arusha city kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Arusha, Nindwa Maduhu amesema uwanja huo utajengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 9.6 na utakuwa na uwezo wa kubeba watazamaji 8,000 waliokaa.

Sauti ya Nindwa Maduhu, Mwakilishi wa Mkurugenzi