Savvy FM

Laigwanan kupasua chungu waliopora ardhi yao

June 2, 2025, 2:43 pm

Leskari Olobisi, Mwenyekiti Kitongoji cha Esilalei akizungumza na waandishi wa habari. Picha na Fredrick Lyimo

Wananchi wa kijiji cha Engutukoit kata ya Oldonyowas wametoa siku 7 kupasua chungu kwa ajili ya watu wote wanaotaka kuwapora eneo la ardhi kwa ajili ya malisho ya mifugo yao.

Na Juliana Laizer

Wakizungumza katika mkutano ambao mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Wilaya ambaye aliwakilishwa na Naibu Katibu Tawala wa Arumeru Bw. Japhet Nguirana wenyeviti wa vijijiji hivyo wameleza kuwa serikali ya kijiji kupitia Mtendaji wamefoji muktasari wa uongo ambao lengo ni kuwapora ardhi kwa ajili ya malisho.

Sauti ya Leskari Olobisi,Mwenyekiti Kitongoji cha Esilalei

Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji cha Engutukoit Loserian Paangu ameiomba serikali kutatua tatizo hilo la mgogoro wa ardhi ili wananchi wake wasiendelee kuteseka

Sauti ya Loserian Paangu Mwenyekiti wa kijiji cha Engutukoit

Kutokana na sintofahamu hiyo mgeni rasmi ndugu Japhet Nguirana ambaye ni Katibu Tawala Wilaya ya Arumeru amewashukuru kwa kikao na kuahidi kuyafikisha malalamiko yao kwa Mkuu wa Wilaya.

Sauti ya Japhet Nguirana,Katibu Tawala Wilaya ya Arumeru.mp3