Savvy FM

Jamii ya kimasai yasafirishwa hadi Kenya kujifunza hewa ukaa

April 30, 2025, 5:47 pm

Lekoko Ngotiek-Mratibu wa shirika la soil for the feature Wilaya ya Monduli.Picha na Juliana Lizer

Shirika la soil for the feature linalojishughulisha na biashara ya hewa ukaa limewasafirisha baadhi ya wananchi na viongozi wa vijiji na kata katika Wilaya za Monduli na Longido hadi Kajiado nchini Kenya ili kupatiwa elimu ya namna ya biashara hiyo inavyofanyika katika nyanda za malisho.

Na Juliana Lizer

Wakizungumza mara baada ya mafunzo hayo wananchi hao wamesema walichojifunza na kujionea zaidi ni namna uvunaji wa hewa ukaa unavyofanyika katika nyanda za malisho bila kuathiri kitu chochote

Lekoko Ngotiek ni mratibu wa mradi wa carbon wilayani Monduli amezungumzia makubaliano waliyokubaliana na jamii ya kimasai hadi kupelekea kuwapeleka nchini Kenya kupata elimu juu ya hewa ukaa