Buha FM Radio

Yaliyojificha kuhusu malezi ya watoto katika jamii

February 25, 2026, 7:01 pm

Afisa Ustawi wa Jamii kutoka Hospitali ya Wilaya ya Kasulu Mlimani Virginia Frednand akieleza jinsi jamii inavyopaswa kushirikiana katika malezi ya watoto. Picha na Sharifat Shinji.

“Watoto wamefikia sehemu wanajichukulia maamuzi yao jambo linalosababishu kuzalisha majambazi, vibaka, watoto wamtaani jamba ambalo sio zuri na sisi kama ustawi wa jamii tunaendelea kutoa elimu katika jamii na kuwasisitiza kushirikiana katika malezi” Amesema Virginia Fredinand.

Na; Emily Adam

Baadhi ya wazazi katika Wilaya ya Kasulu wametaja sababu zinazopelekea kushindwa kushirikiana katika malezi ya watoto jambo lilalopelekea mmomonyoko wa maadili kwa kizazi kilichopo na kijajcho.

Kwa muujibu wa Majapisho mbalimbali Ulimwengu likiwemo chapisho la Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wanawake na Makundi Maalumu imeeleza jinsi jamii ilivyo na mchango mkubwa katika malezi ya watoto Makala ya kipindi chetu leo imeelaza kinaga ubaga jinsi Jamii inavyopaswa kushiriki katika malezi ya watoto.