Buha FM Radio
Buha FM Radio
September 10, 2025, 7:29 am

“Elimu ya Kipindupindu tunaendelea kuitoa kwa wananchi kupitia vyombo vya habari kutokana na ongezeko la maambukizi ya ugonjwa huu ambapo mwezi Augost kulikuwa na visa vitatu hadi leo Septemba 08 mwaka huu vimefikia visa 37 vya maambukizi ya ugonjwa huu hivyo wananchi wachukuwe tahadhari kubwa” Amesema Mwita.
Na; Paulina Majaliwa
Kutokana na kuenea kwa mlipuko wa ugonjwa wa Kipindipindu kwa baadhi ya maeneo Halmashauri ya Mji Kasulu mkoani Kigoma wakulima wameshauriwa kuchukua tahadhari juu ya ugonjwa huo kwani eneo lenye uwezekano mkubwa wa kupata ugonjwa huo.
Hayo yamebainishwa na mratibu wa elimu ya afya kwa umma Halmashauri ya Mji Kasulu ndg. Mwita Range wakati akizungumza na Buha FM kupitia kipindi cha darasa nje ya shule ambapo amesema wakulima wengi wanatumia vyakula vya baridi pamoja na maji yasiyosafi na salama kutoka kwenye visima au madimbwi na pia kujisaidia vichakani.
Aidha Mwita amesema kundi kubwa linaloshambuliwa na kipindupindu ni wakulima hii ni kutokana na hali ya mazingira wanayofanya kazi zao kuwa si rafiki kwa afya zao.

Pia amewataka wakulima hao kuwahi katika kituo cha afya pale mtu anapopatwa na dalili za kipindupindu kama kutapika na kuharisha kusiko kawaida ili kuokoa maisha yao na kuepusha kusambaa kwa ugonjwa.
“Kuna baadhi ya watu wamekuwa wakipatwa na dalili za ugonjwa huu wanachukulia jambo la kawaida jambo linapelekea mtu kupatwa na umauti kutokana na kuchelewa kupata huduma hivyo niwaombe wananchi wachukue tahadhari mapema’’amesema Mwita.
Mtaalamu ameelekeza kuwa katika Halmashauri ya Mjii Kasulu kituo cha afya kinachotumika kutibu wagonjwa wa kipindupndi ni kituo cha afya Nyasha hii ni kutokana na kituo hicho kimewekwa maalum kwa kutibu wagonjwa wanaopatikana na ugonjwa huo.
Amehitimisha kwa kuwataka wananchi kujiepusha na kukimbilia tiba za asili kwani hii imekuwa ni sababu ya watu wengi kupoteza maisha yao kutokana na kuanzia kwa waganga wa kienyeji bila kufuata taratibu za kitaalamu.
Kwa mujibu wa mratibu wa elimu ya afya kwa umma halmashauri ya mji kasulu Ndg. Mwita Range amesema mpaka kufikia Septemba 08,mwaka huu takwimu zinaonyesha kuwa takribani visa 37 vya ugonjwa wa kipindupindu vimepatikana vifo 05 na waliotibiwa na kuruhusiwa ni watu 29 kutoka maeneo mbalimbali ya kata za Halmashauri ya Mji Kasulu Mkoani Kigoma.