Buha FM Radio

Prof. Masanja: Tumia mbolea sahihi shambani kwako

July 24, 2025, 10:28 pm

Mbolea ya samadi. Picha na Irene Charles

Kuna aina tatu za mbolea ambazo ni mbolea za Samadi (kinyesi cha Mnyama au ndege) ambazo zinamatikana kwa urahisi majumbani, Mbolea zinazotoka viwandani na mbolea inayotokana na masalia ya mimea, mabaki ya samaki pamoja na mifupa ya ndege.

Na Irene Charles

Kila mkulima ana jukumu la kujua ni mbolea gani anapaswa kutumia shambani ambayo italeta matokeo mazuri na kusaidia kizazi na kizazi kutumia ardhi hiyo na si kila mbolea na inapaswa kuwekwa shambani.

Hayo yamesemwa leo na Afisa kilimo Prof. Masanja wakati akizungumza na Buha FM Redio na kusema mkulima anapaswa kufahamu ni aina gani ya mbolea anatumia kulingana na ardhi yake kwa lengo la kulinda ardhi hiyo.

Sauti ya Afisa Kilimo Prof. Masanja.

Aidha Prof. Masanja amewashauri wakulima kutumia mbolea kiasi cha mfuko wa kilo 50 kwa kupandia na mfuko wa kilo 50 kwaajili ya kukuzia mazao kwa ekari moja lakini kwa mkulima wa nyumbani kifuniko kimoja cha maji kwa kila shina.

Sauti ya Afisa Kilimo Prof. Masanja.

Hata hivyo Prof. Masanja amesema mkulima ambaye hatatumia mbolea ambayo sio sahihi atasababisha uharibu wa aridhi lakini pia mmea kudhohofika na hivyo kupata mavuno kwa kiwango cha chini.  

Kwa mujibu wa Prof. Masanja kuna aina tatu za mbolea ambazo ni mbolea za Samadi (kinyesi cha Mnyama au ndege) ambazo zinamatikana kwa urahisi majumbani, Mbolea zinazotoka viwandani na mbolea inayotokana na masalia ya mimea, mabaki ya samaki pamoja na mifupa ya ndege.