Buha FM Radio

Wadau washiriki zoezi la usafi siku ya Uhuru

April 24, 2025, 2:51 am

Baadhi ya watumishi wa serikali wakifanya usafi katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji Kasulu. Picha na Shinji.

Katibu tawala Bi, Theresia Mtewele awapongeza waote walioshiriki zoezi la usafi katika maeneo yote wilayani Kasulu.

Katika kuadhimisha miaka 63 za Uhuru wa Tanganyika Leo Decemba 9 Buha fm radio ilifika katika Hospital ya Halmashauri ya Mji Kasulu ambako kulikuwa na zoezi la usafi wa mazingira ikiwa ni sehemu ya Utekerezaji wa akizo la Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhusu kuadhimisha siku ya Uhuru wa Tanganyika

 Katibu tawala wa wilaya ya Kasulu Bi, Theresia Mtewele Ameshiriki katika zoezi la usafi katika Hospitali Ya Halmashauri ya Mji Kasulu huku akipongeza zoezi hilo baada kukamilika.

Sauti ya katibu tawala wilaya ya Kasulu Bi, Theresia Mtewele.
Katibu tawala wilaya ya kasulu akiendelea na zoezi la usafi katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji Kasulu. Picha na Shinji.

Aidha Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji Kasulu Mwalimu Vumilia Simbeye amezungumza mara baada ya Zoezi la usafi  katika hospitali hiyo huku akisema zoezi hilo ni kuboresha mazingira hospitali hiyo. 

Sauti ni Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji Kasulu Mwalimu Vumilia Simbeye.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kasulu Mwalimu Vumilia Simbeye akifyeka nyasi siku ya Uhuru wa Tanganyika. Picha na Shinji.

Kwa Upande wa Jeshi la polis wilaya ya kasulu limeshiriki katika zoezi hilo huku  Mkuu wa Jeshi la Polisi SSP SANGO amesema jeshi la polisi linajukumu la kushirikiana na wanachi katika zoezi hilo ili kuweka mazingira salama.

Sauti ya Mkuu wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Kasulu SSP SANGO.

Zoezi la usafi limefanyika katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji Kasulu likiwa na kauli Mbiu ya UONGOZI MADHUBUTI NA USHIRIKISHWAJI NDO MSINGI WA MAENDELEO YETU ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 63 ya Uhuru wa Tanaganiyika huku Halmaashauri ya Kasulu vijijini zoezi hilo limefanyika katika Hospitali ya wilaya hiyo likiwa limeambatana na uchangiaji wa Damu.

Pichani ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kasulu Mwalimu Vumilia Simbeye na Mkuu wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Kasulu SSP SANGO.