Savvy FM

Sitokamilika kama sitowahusisha viongozi wa dini-RC Makalla

September 1, 2025, 3:48 pm

Picha ya pamoja ya viongozi wa Bakwata Mkoa wa Arusha na Mkuu wa mkoa wa Arusha Amos Makalla.Picha na Jenipha Lazaro

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Amos Makalla, ameanza rasmi ziara yake ya kikazi mkoani hapa kwa kutembelea taasisi mbalimbali za kidini, akianza na Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) ambapo ametoa wito kwa viongozi wa dini kuendelea kushirikiana na serikali katika kuleta maendeleo kwa wananchi.

Na Jenipha Lazaro

Akizungumza katika Ofisi za BAKWATA zilizopo katika msikiti mkuu wa Ijumaa, Bondeni, RC Makalla amesema kuwa serikali inatambua na kuthamini nafasi ya viongozi wa dini katika jamii, hasa katika kipindi hiki ambapo nchi inaelekea kwenye uchaguzi.

Sauti ya Amos Makalla,Mkuu wa Mkoa Arusha

Naye Sheikh wa Mkoa wa Arusha, Sheikh Shaban Abdala, alimhakikishia Mkuu wa Mkoa kuwa viongozi wa dini wataendelea kuwa wadau wakuu wa maendeleo katika kila awamu ya uongozi wa serikali

Sauti ya Sheikh Shaban Abdala,sheikh wa mkoa wa Arusha

Kwa upande wake, Katibu wa BAKWATA Mkoa wa Arusha, ndg. Ali Nassor, alieleza kuwa taasisi hiyo imejipanga kutumia maadhimisho ya sikukuu ya Maulid kama jukwaa la kuhubiri na kutangaza amani, hasa kipindi hiki cha uchaguzi, kwa kushirikiana na serikali

Sauti ya Ali Nassor,Katibu BAKWATA