Bunda FM Radio

Bunda Quuens yaendelea kujifua kuelekea msimu mpya wa ligi kuu

September 12, 2025, 7:14 pm

Kocha mkuu wa Bunda queens Aley Ibrahimu akizungumzia maandalizi ya timu yake kwelekea msimu mpya wa ligi kuu ya wanawake 2025/2026. Picha na Simon Maryogo Yusuph

“Tuna malengo ya kufanya vizuri msimu ujao na kushika nafasi ya nne za juu ili tupate nafasi ya kucheza ngao ya jamii’’ Kocha mkuu wa Bunda queens Aley Ibrahimu

Na Amos Marwa

Timu ya soka ya wanawake Bunda Queens  inayoshiriki ligi kuu ya wanawake Tanzania bara imeendelea na mandalizi ya msimu mpya kwa kufanya mazoezi katika uwanja wa shule ya msingi Miembeni wilayani Bunda.

Akizungumza na Bunda FM , Baada ya maozoezi ya asubuhi uwanjani hapo kocha mkuu wa timu hiyo Aley ibrahimu amesema maandalizi yanaendelea vizuri na anaamini vijana wake watafanya vizuri katika msimu mpya wa 2025/2026.

Sauti ya kocha mkuu wa Bunda queens Aley Ibrahimu akizungumzia maandalizi ya timu hiyo kwelekea msimu ujao.

Aidha, ameongeza kuwa wameondokewa na  wachezaji wake watatu akiwemo Ester Maseke alietimkia Jkt quuens waliokuwa tegemeo katika kikosi hicho lakini timu hiyo imesajili wacheza wa kuchukua nafasi zao na watafanya vizuri, kwani wamesajili wachezaji bora na kupandisha wachezaji wengine kutoka timu ya vijana.

Sauti ya kocha mkuu wa Bunda queens Aley Ibrahimu akizungumzia wachezaji waliondoka akiwemo Ester Maseke na waliokuja kuchukua nafasi zao.

Kwa upande wake nahodha wa timu hiyo Jamila Celestine kwa niaba ya wachezaji wenzake amesema wamejiandaa vizuri kukabiliana na mikikimikiki ya ligi hiyo na kuwaomba mashabiki kujitokeza kwa wingi katika michezo yao kwa ajili ya kuwapa hamasa.

Sauti ya nahodha wa Bunda queens Jamila Celestine akielezea maandalizi ya timu hiyo kwa niaba ya wachezaji wenzake.

Msimu uliyopita timu ya Bunda queens ilimaliza ligi katika nafasi ya  6 ikiwa  imejikusanyia jumla ya alama 19 baada ya kushuka dimbani michezo 16 wakishinda michezo 5 wakisare michezo 4 na kupoteza michezo  7.

Nahodha wa timu ya Bunda queens Jamila Celestine akielezea maandalizi yao kwa niaba ya wachezaji wenzake kwelekea msimu mpya wa ligi kuu ya wanawake 2025/2026. Picha na Simon Maryogo Yusuph