Bunda FM Radio

Timu ya Bunda Girls yaelekea Mwanza kushiriki mashindano ya ligi daraja la kwanza

June 7, 2025, 10:32 am

Mkuu wa wilaya ya Bunda Aswege Enock Kaminyoge (mwenye miwani) akiwaaga viongozi na wachezaji wa Bunda Girls wanaoelekea Mwanza kwenye mshindano ya ligi daraja la kwanza. Picha na Amos Marwa

Mkacheze kufa ama kupona ili muweze kufuzu kwenda ligi kuu ya wanawake kwasababu mnawakilisha wilaya ya Bunda na Mkoa wa mara kwaujumla” Mkuu wa Wilaya ya Bunda Aswege Enock Kaminyoge

Na Amos Marwa

Mkuu wa wilaya ya Bunda Aswege Enock Kaminyoge amewataka wanamichezo kuongeza jitihada katika mazoezi na michezo kwa ujumla kwa kuwa michezo inaimarisha Afya na ni ajira kwa vijana.

Amesema hayo wakati akiwaaga wachezaji na viongozi wa timu ya Bunda Girls inayoelekea jijini Mwanza kushiriki mashindano ya ligi daraja la kwanza yatakayo wawezesha kufuzu katika hatua ya ligi kuu ya wanawake msimu ujao na kuwaomba waongeze jitihada ili waweze kufuzu.

Sauti ya Mkuu wa wilaya ya Bunda Aswege Enock Kaminyoge akiwatakia heri wachezaji na viongozi wa timu ya Bunda Girls kwelekea jijini Mwanza kushiriki mashindano hayo
Mkuu wa wilaya ya Bunda Aswege Enock Kaminyoge aliesimama katikati akizungumza na wachezaji na viongozi wa timu ya Bunda Girls

Kwa upande wake Mwenyekiti wa timu hiyo Khalid Shani amesema wamepata muda mrefu wa kuandaa wachezaji na kuahidi mashabiki na wapenzi wa soka mkoa wa Mara kuwa watafuzu katika mashindano hayo.

Sauti ya Mwenyekiti wa timu hiyo Khalid Shani akielezea maandalizi yao kwelekea jijini mwanza.
Kocha wa Timu ya Bunda Girls Emanuel Simion akielezea walivojipanga kiufundi katika mashindano hayo. Picha na Amos Marwa

Kocha wa timu hiyo Emmanuel Simion amesema timu imejiandaa vizuri kiufundi na amefuatilia wapinzani wao kwa ajili ya kukabiliana nao huku akiomba mashabiki na wadau wa soka kwendelea kuwaunga mkono.

Sauti ya Kocha wa Bunda Girls Emanuel siomion akizungumzia maandalizi yao kiufundi na kuomba mashabiki kuunga mkono timu hiyo.
Nahodha wa timu ya Bunda Girls Angel Bahati akielezea maandalizi yao kwa niaba ya wachezaji wa timu hiyo. Picha na Amos Marwa

Nae, Nahodha wa timu hiyo Angel bahati amesema kwa niamba ya wachezaji wenzake wamejiandaa vizuri na kuwatoa hofu mashabiki wa timu hiyo kuwa watafanya vizuri.

Sauti ya Nahodha wa timu ya Bunda Girls Angel Bahati kwa niaba ya wachezaji wenzake akiwa hofu mashabiki wa timu hiyo kwelekea mashindano hayo.

Mashindano hayo yanatarajia kuanza juni 8 , 2025 jijini Mwanza na timu nne kupanda kutoka ligi daraja la kwanza na kuingia ligi kuu ya wanawake kwa msimu wa mwaka 2025/2026