Bunda FM Radio

Madiwani Bunda Mji watakiwa kushirikiana na wakuu wa idara ya elimu

May 21, 2025, 11:50 am

Katibu tawala Wilaya ya Bunda Salum Khalfan Mtelela akizungumza na madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Bunda katika kikao cha mwisho cha baraza la madiwani. Picha na Amos Marwa.

”Madiwani shirikianeni na watendaji wa mitaa pamoja na wazazi ili kuhakikisha upatikanaji wa chakula cha mchana kwa ajili ya wanafunzi wa shule za Msingi na Sekondari”, Salum K. Mtelela katibu tawala Wilaya ya Bunda.

Na Amos Marwa

Katibu tawala wa wilaya ya Bunda Salum  Alfan Mtelela amewataka Madiwani washirikiane na wakuu wa idara ya elimu kuhakikisha upatikanaji wa Chakula mashuleni ili kuongeza ufaulu kwa Wanafunzi wa shule za msingi na sekondari.

Akiwasilisha salamu za Serikali katika Baraza la Madiwani lilofanyika kwenye Ukumbi wa Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bunda Mtelela amesema wilaya ya Bunda ni moja ya wilaya zinazofanya vizuri katika suala la chakula mashuleni na inapaswa kuongeze nguvu katika suala hilo.

Sauti ya katibu tawala Wilaya ya Bunda Said Khalfan Mtelela akizungumza kuhusu upatikanaji wa chakula

Aidha katibu tawala  amesema  kuwa pamoja na jitihada za serikali kuimarisha miondombinu katika mashule pia ameongeza kuwa suala la madili kwa wanafunzi ni la kutiliwa mkazo ili kuondoa  nidhamu mbovu kwa wanafunzi ikiwemo matumizi ya Simu mashuleni na vitendo vya mapenzi ya jinsi moja.

Sauti ya katibu tawala Wilaya ya Bunda Saluk Khalfan Mtelela akizungumza kuhusu maadili ya wanafunzi mashuleni.

Kwa upande mwingine baraza la madiwani la Halmashauri ya Mji wa Bunda   limejadili kuhusu Malipo ya Posho kwa Wenyeviti wa Serikali za Mitaa, ujenzi wa Soko la Bunda mjini,  ujenzi wa Zahanati mbalimbali na changamoto za upatikanaji wa maji kwa Wananchi katika halmashauri ya Mji wa Bunda.

Baadhi ya madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Bunda wakiwa katika kikao cha baraza. Picha na Amos Marwa.