Buha FM Radio
Buha FM Radio
6 Aprili 2026, 09:51

Wananchi wilayani Kasulu na mkoa wa Kigoma kwa ujumla waombwa kujitokeza siku ya kambi ya madaktari bingwa katika hospitali hiyo.
Na; Sharifat Shinji
Hospitali ya Rufaa Kabanga wilayani Kasulu mkoani Kigoma inatarajia kuwa na Kambi ya madaktari bingwa kuanzia tarehe 13 hadi 17 mwezi April, 2026 kwa lengo la kuwasaidia wakazi wa Mkoa wa Kigoma na maeneo jirani wenye changamoto mbalimbali za kiafya.
Hayo ameyasema Afisa mahusiano wa hospitali hiyo Bi. Neema Mwaipopo wakati akizungumza kwa niaba ya Mganga mfawidhi wa Hospitali Dkt. Peter Kitenyi, ambapo amesema kambi hiyo itawezesha utoaji wa huduma mbalimbali za kibigwa kwa wananchi wote wa Wilaya ya Kasulu na maeneo jirani.
Aidha Mwaipopo amesema hospitali inapokea na kutoa huduma kwa wagonjwa wote wenye bima na wasio na bima huku akiwakaribisha wananchi waote wa Wilaya ya Kasulu kujitokea kupata huduma za kibingwa katika hospitali hiyo.

Hospitali ya Rufaa Kabanga huwa inaandaa Kambi ya madaktari Bingwa kila mwezi kwa lengo la kuwahudumia wananchi wenye changamoto mbalimbali za matibabu ya kibingwa, kambi hiyo huandaliwa na hospitali ya Kabanga kwa kushirikiana na madakitari bingwa kutoka hospitali ya rufaa Kabanga.