Wananchi Kagerankanda wamlilia mbunge kuhusu migogoro ya ardhi
Buha FM Radio

Wananchi Kagerankanda wamlilia mbunge migogoro ya ardhi

January 5, 2026, 7:06 pm

Baadhi ya wananchi wa kata ya Kagerankanda wakiwa katika mkutano wa hadhara wa Mbunge wa Jimbo la Kasulu Vijijini. Picha Ajomba Lukumba.

Mbunge wa Kasulu vijijini Mhe. Edibily Kazala aneahidi kutatua changamoto zote ilizopo katika kijiji cha Kagerankanda na Jimbo la Kasulu vijijini kwa ujumla.

Na; Mwandishi wetu

Wananchi wa kijiji cha Kagerankanda katika Jimbo la kasulu Vijijini Mkoani Kigoma wamemuomba Mbunge wa jimbo hilo kutatua kero zilizopo ndani ya kijiji hicho ikiwemo mgogoro wa wakulima na wafugaji.

Malalamiko hayo wameyatoa jana kijijini hapo wakati wa mkutano wa hadhara wa mbunge wa jimbo hilo na kusema licha ya uwepo wa mgogoro huo bado kijiji hicho kinakumbwa na changamoto za huduma ya afya kutokana na wajawazito kutozwa fedha wakati wa kujifungua.

Sauti za baadhi ya wananchi wa Kagerankanda.

Kwa upande wake Mbunge wa jimbo hilo Edibily Kazala ameahidi kutekeleza ahadi zote alizoziahidi katika kipindi cha kampeni ikiwa ni pamoja na kutatua migogoro ya ardhi hasa katika eneo la Katoto lililouzwa kinyume na taratibu za kisheria.

Sauti ya Mbunge wa Kasulu Vijijini Edibily Kazala.

Aidha Mbunge huyo ameongeza kwa kusema  ameanza mchakato wa kuhakikisha barabara za lami zilizopo katika mpango wa serikali zinajengwa na kukamilika kwa wakati ili kuinua uchumi wa wananchi wa kijiji hicho.

Sauti ya Mbunge wa Kasulu Vijijini Edibily Kazala.

Mbunge wa Kasulu Vijijini Edibily Kazala akiwa anazungumza na wananchi wa Kagerankanda katika Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu. Picha Ajomba Lukumba.