Buha FM Radio

Kwashayo yatajwa sababu mdororo wa wateja Mnadani

September 19, 2025, 5:33 pm

Muonekano wa jengo la soko la Mazao Mnadani amabalo halijaanza kutumiwa na wafanya biashara. Picha na Paulina Majaliwa.

“Kiukweli uwepo wa soko la Kwashayo inatufanya sisi tushindwe kupata wateja serikali ikamilishe soko hili wafanya biashara waliopo kule wahamie hapa maana wakiwepo kule sisi hatuuzi kabisa hali hii inapelekea kushindwa hata kuendesha familia zetu” Alisikika mmoja ya wafanya biashara akizungumza.

Na; Irene Charles

Baadhi ya Wafanya biashara wa mazao katika soko Mazao Mnadani lililopo Halmashauri ya Mji Kasulu mkoani Kigoma wamesema hali ya  ngumu ya mauzo   mahindi imekuwa ni changamoto kwao kutokana na uwepo wa soko la Kwashayo hali inayopelekea uchaje wa wateja katika soko hilo.

Wamebainisha   hayo walipotembelewa na Buha FM radio Kutaka kufahamu hali ya mauzo katika soko hilo na kuiomba serikali kukamilisha ujenzi wa soko ili iwasaidie kuongeza na kurahisisha upatikaji wa wateja wa kutosha katika maeneo yao ya biashara.

Sauti za wananchi wakizungumzia kuhusu soko la Mnadani.

Eshodi Rajabu ni mfanyabiashara wa nafaka za mahindi na maharage amesema upatikanaji wa mahindi kwa sasa ni mzuri lakini changamotoo ni masoko kwani hawana wateja wa kudumu katika soko hilo.

Sauti ya Eshodi Rajabu ambaye ni Mfanyabiahara katika Soko la Mazao mnadani.
Eshodi Rajabu mfanyabiahara wa nafaka katika soko la mazao mnadani.Picha na Paulina Majaliwa.

Aidha katibu wa wafanyabiashara katika soko la mazao Mnadani ndug.Nelson Msyomole  amesema serikali kupitia mkurugenzi wa  Halmashauri ya Mji Kasulu  wamesema mpaka kufika mwezi wa 12 ujenzi wa soko jipya  utakuwa umekamalika.

Sauti ya Katibu wa wafanyabiashara katika soko la mazao Mnadani ndug.Nelson Msyomole.

Katika hatua nyingine Bw.Nelson amesema baada ya soko la Mnadani kukamilika  wafanyabiashara wa soko la Kwashayo watahamia katika soko jipya kwa sababu litakua linatabulika kisheria,huku akiwaasa kufanya usafi kila siku katika maeneo yao ya biashara.

Sauti ya Katibu wa wafanyabiashara katika soko la mazao Mnadani ndug.Nelson Msyomole.

Kwa muujibu wa kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika Desemba 11, 2024 kilijadili kuhusu usitishwaji wa soko la Kwashayo kufanya shughuri za biashara majira ya asubuhi na kulipa uhalali soko hilo majira ya saa 12 jioni baada ya soko la Mazao Mnadani kufungwa lakini hadi sasa masoko yote mawili yanafanya kazi kwa masaa sawa hali inayopelekea soko la Mnadani kuwa na Mdororo wa wateja hali inayopelekea wafanya biashara kushindwa kuendesha shughuli za biashara katika soko hilo.

Muonekano wa baadhi ya Biashara za mahindi katika soko la mazao Mnadani. Picha na Paulina Majaliwa.