Buha FM Radio

Walimu Msambala sekondari wakabidhiwa nyumba ya two in one 2-1

September 18, 2025, 10:18 pm

Kiongozi wa Mbio za Mwenge kitaifa Ndg. Ismail Ussi akizungumuzia namna Serikali inavyotekeleza miradi kwa upande wa idara ya Elimu. Picha na Sharifat Shinji.

“Serikali kupitia kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuwajali wadau wa elimu na idara ya elimu kwa ujumla katika kutekeleza miradi itakayosaidia kuongeza ufaulu kwa wanafunzi na kuwatengenezea walimu mazingira mazuri ya kufundishia” Amesema Ndg. Ussi.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge kitaifa Ndg. Ismail Ussi amezindua nyumba ya walimu  two in one 2_1 katika shule ya sekondari Msambala katika Halmashauri ya Mji Kasulu nyumba itakayowasaidia watumishi kufundisha wakiwa katika makazi bora ya kuishi.

Uzinduzi huo umefanyika Leo Septemba 18 katika Eneo la Shule hiyo ikiwa ni mwendelezo wa mbio za Mwenge wa Uhuru katika  Halmashauri ya Mji Kasulu mkoani Kigoma huku kiongozi wa mbio za mwenge  akiwasisitiza walimu kutunza miundombinu yote inazotekelezwa na serikali mkuu.

Sauti ya kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa.

Aidha Ussi amekipongeza kitengo cha kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU kwa kuendelea kutoa elimu kwa wanafunzi wa shule za sekondari, msingi na vikundi mbalimbali ikiwemo wajasiliamali na Maafisa usafirishaji maalufu Bodaboda kwa kuunda vikundi vya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU ili kutokomeza tatizo la rushwa nchini.

Sauti ya kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa.
Mkuu wa Wilaya Mhe. Kanali Isack Mwakisu akitoa maelezo kuhusu nyumba ya watumishi shule ya sekondali Msambala. Picha na Sharifat Shinji.

Awali akisoma taarifa ya ujenzi wa nyumba hiyo Mkuu wa shule ya sekondari Msambala Mwl. Werema  Mashenene kwa niaba ya Mkurugenzi mtendaji Halmashauri ya Mji  amesema mradi huo umegharimu Million 110 hadi kukamilika.

Sauti ya Mkuu wa shule ya sekondari Msambala Mwl. Werema  Mashenene.
Mkuu wa shule ya sekondari Msambala Mwl. Werema  Mashenene akisoma taarifa ya mradi wa nyumba ya watumishi two in one shule ya sekondari Msambala. Picha na Sharifat Shinji.

Sanjari na uzinduzi na kuweka Jiwe la msingi la nyumba ya walimu katika Shule hiyo, pia Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa amezindua na kuweka jiwe la msingi la klabu ya wanafunzi ya kupambana  na kuzuia Rushwa  TAKUKURU katika shule hiyo yenye wanachama zaidi ya 100 katika shule hiyo.

Kiongozi wa mbio za mwenge Kitaifa akiwa na viongozi wa serikali na chama wakizindua nyumba ya walimu Katika shule ya sekondari Msambala. Picha na Sharifat Shinji.