Buha FM Radio

Dkt. Suzana: Bawasiri sio laana wala aibu

July 8, 2025, 6:11 pm

Dkt. Suzana wakati akiongea na Buha FM Radio. Picha na Irene Charles

Ili kuepukana na ugonjwa wa bawasiri suluhisho kwa kunywa maji ya kutosha angalau kila siku glasi sita au nane kwa siku, kula mbogamboga na matunda, kuepuka kukaa au kusimama sehemu moja kwa muda mrefu na kufanya mazoezi.

Na Irene Charles

Bawasiri sio laana wala sio aibu bali ni ugonjwa unao sababishwa na sababu mbalimbali kama kukaa na kusimama kwa muda mrefu, uzito uliopitiliza, kula kwa wingi nyama nyekundu na vidonda vya tumbo, ngiri na chango.

Hayo yamesema na mtaalamu wa afya ya uzazi Dkt. Suzana Geazi Ngogo kutoka Hemocare Clinic wakati akizungumza na Buha FM Radio ambapo amesema dalili za bawasiri ni kupata muwasho mkali, kujitokeza kinyama sehemu ya aja kubwa pamoja na kupata maumivu makali wakati wa kujisaidia.

Kwa upande wao Baadhi ya wakazi wa Halmashauri ya Mji Kasulu wamesema kuwa hawana uelewa wa kutosha juu ya ugonjwa huo huku wakiwaomba wataalamu wa afya kuendelea kutoa elimu ya kutosha.

Sauti ya Mwananchi.

Ili kuepukana na ugonjwa wa bawasiri Dkt. Suzan amesema suluhisho kwa kunywa maji ya kutosha angalau kila siku glasi sita au nane kwa siku, kula mbogamboga na matunda, kuepuka kukaa au kusimama sehemu moja kwa muda mrefu na kufanya mazoezi.

Sauti ya Dkt. Suzana.

Pia Dkt. Suzan amesema watoto wadogo wanaweza kupata bawasiri hivyo  ameshauri kwa mama anayenyonyesha  kuhakikisha anakula matunda, chakula cha kutosha pamoja na maji ya kutosha ili kumkinga mtoto dhidi ya ugonjwa huo.

Sauti ya Dkt. Suzana.