Buha FM Radio

Lucy Samson: Mwanamke simamia nafasi yako

June 27, 2025, 10:52 am

Mwl. Lucy Samsoni Katibu wa idara ya wanawake Taifa katika kanisa la Babtisti Tanzania. Picha na Mbaraka Shabani

Baadhi ya wananchi walioshiriki katika mkutano huu wameshukuru kwani mkutano umemalizika kwa amani lakini umewafundisha mambo mengi ikiwa pamoja na kukaa na familia na kulea watoto katika maadili mazuri yanayohitajika katika jamii.

Na Irene Charles

Katibu wa idara ya wanawake taifa katika kanisa la Babtisti Tanzania mwl. Lucy Samsoni ametoa wito kwa wanawake kumtumikia mungu kwani  nafasi ya mwanamke ni kubwa sana ambayo mungu ameweka ndani yake. Amesema hayo katika  mkutano wa kanda wa idara ya wanawake uliyofanyika  kanda ya magharibi kata Buhoro amesema mwanamke akisimama  katika nafasi yake kuanzia ngazi ya familia  lazima mambo yatimie.

Sauti ya Mwl. Lucy Samsoni Katibu wa idara ya wanawake Taifa katika kanisa la Babtisti Tanzania.

Kwa upande wake katibu wa kanisa la Babtisti  nyamsanze kata ya Buhoro ndg. Selemani Balagwana ameushukuru umoja wa wanawake kwa kutambua pia uwepo wao na kuwakaribisha pia wanaume katika mkutano huu hata kuchangia mawazo ya kiinjili ili kujenga jamii yenye umoja.

Sauti ya Katibu wa kanisa la Babtisti  Nyamsanze kata ya Buhoro Selemani Balagwana.

Nao baadhi ya wananchi walioshiriki katika mkutano huu wameshukuru kwani mkutano umemalizika kwa amani lakini umewafundisha mambo mengi ikiwa pamoja na kukaa na familia na kulea watoto katika maadili mazuri yanayohitajika katika jamii.

Mkutano huo ulikuwa na lengo la kuwasaidia wanawake kujiinua kiuchumi na malezi katika familia ambapo kwa kanda ya magharibi inajumuisha mkoa wa Kigoma, Katavi na Tabora kwa mwaka 2025 umefanyika katika kanisa la Babtisti Nyamsanze Buhoro.