Buha FM Radio

Wazazi na walimu sasa kujenga madili bora ya mwanafunzi

June 4, 2025, 9:31 pm

Baadhi ya wazazi katika Halmashauri ya Mji Kasulu wajipanga kushilikiana na walimu kulinda na kujenga madili bora kwa wanafunzi ili kuendelea na taifa lenye raia wenye madili bora.

Na: Paulina Majaliwa

Baadhi ya wazazi katika Halmashauri ya  Mji Kasulu mkoani Kigoma wamewaomba walimu kushirikiana na wazazi katika kuimarisha maadili na malezi ya wananfunzi wanapokuwa shuleni.

Wameyasema hayo wakati wakizungumza na Buha FM radio ambapo wamesema kuwa shule ni moja ya sehemu ambayo mtoto anapata maadili mema na malezi mazuri hivyo wamesema ni wajibu wa wazazi na walimu katika kujenga jamii yenye maadili mema.

Baadhi ya sauti za wazazi katika Halmashauri ya Mji Kasulu wakizungumzia maadili kwa wanafunzi.

Aidha wamesema kuwa wanafunzi wanatakiwa kuwaheshimu walimu kama wanavyo waheshimu wazazi wao wawapo majumbani kwani walimuni watu wanaowasaidia  wazazi  katika malezi ya Watoto ili kuimarisha maadili katika jamii.

“Tunawashukuru sana walimu wanatusaidia kuwalea watoto wetuwanapokuwa shuleni kikubwa tuwaombe wanafunzi wawe na nidhamu na wawaheshimu walimu kama wanavyotuheshimu sisi wanapokuwa nyumbani” Amesema miongoni mwa wazazi hao.

Kwa upande wake makamu mkuu wa shule ya msingi na awali Kalinone iliyopo wilayani Kasulu Mwl.Eston Emanuel Edward amesema kuwa malezi shuleni ni miongoni mwa vipengele vinavyozingatiwa na walimu wote hivyo kila shule inaundwa na kamati ya maadili na malezi ili kuwaweka wanafunzi katika misingi inayotakiwa  wawapo shuleni na hata wanapokuwa nyumbani.

Sauti ya makamu mkuu wa shule ya msingi na awali Kalinone Mwl.Eston Emanuel Edward.
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya awali na msingi Kalinone wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kutembelewa na kituo cha radio cha Buha FM. Picha na Mbaraka Shaban.

Katika hatua nyingine wazazi wameomba uongozi wa shule kuwakanya baadhi ya walimu wanaojaribu kuvunja maadili yao kwani wanafunzi wanajifunza jinsi ya kuishi katika jamii kulingana na kile wanachokiona kutoka kwa walezi, pamoja na walimu wao.