Buha FM Radio
Buha FM Radio
May 24, 2025, 10:24 pm

Wakazi wa kata ya Kagerankanda katika halmashauri ya Wilaya ya Kasulu wameombwa kuendelea kushirikiana na viongozi ili kukamilisha kwa haraka zoezi la ujenzi wa kituo cha afya cha kimkakati katika eneo hilo.
Na: Sharifat Shinji
Mganga mkuu katika Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma Dkt. Chacha Tubet amewashukuru wananchi wa Kijiji cha Kagerankanda kwa kujitolea katika zoezi la uandaji wa eneo la ujenzi wa kituo cha afya katika Kijiji hicho na kuwaomba kuendelea kujitolea na kushirikiana na viongozi wa serikali za mitaa.
Ameeleza hayo wakati alipotembelea katika eneo la ujenzi wa kituo cha afya katika Kijiji cha Kagerankanda na kuwaeleza wananchi wa Kijiji hicho kuwa taratibu zote zimeshafanyika za kupata pesa ili ujenzi uanze mara moja.
Aidha Dkt. Tubet amewaeleza wananchi namna wataalamu wa wajengo watakavyopangilia kituo kicho kikae kwa mpangilio upi huku akiwasisitiza kuendelea kushirikiana na viongozi ili kuhakikisha zoezi hilo linakamilika katika hatua za awali itakapofika June 30 mwaka huu.

Kwa upande wake Mtendaji wa Kijiji cha Kagerankanda Ndg. Sebas Bonifas ameeleza mbele ya Mkganga mkuu wa Halmashauri ya Wilaya hiyo shughuli zilizofanywa na wananchi katika kuhakikisha eneo la kujenga kituo cha afya linakamilika Pamoja na ukusanyaji wa mawe kwa ajiri ya utekelezaji wa ujenzi huo kwa kutumia nguvu ya wananchi wa eneo hilo.
Kata ya Kagerankanda imekuwa ikikabiliwa na changamoto ya vituo vya afya Pamoja na zahanati katika maeneo hayo na kupelekea kutembea umbali mrefu kufata huduma za afya, hivyo serikali imejipanga kushirikiana na wananchi ili kuhakikisha kituo cha afya cha kimkakati kinakamilika katika eneo hilo.