Buha FM Radio

Mbio za Mwenge kuzindua miradi ya utekelezaji Kasulu Mji

May 20, 2025, 5:50 pm

Mratibu wa Mbio Mwenge katika halamashauri ya Mji Kasulu Ndg. Daudi Stinga akizungumza na wajumbe wa mwenge mwaka huu. Picha na Sharifat Shinji.

“Kwa mwaka huu tutaendelea kufata vigezo kama ilivyokuwa mwaka jana tutazindua miradi ya afya, Miradi ya elimu, miradi ya Barabara, miradi ya maji na miradi ya mapato ya ndani itakuwemo” Amesema Daudi Stinga.

Na: Sharifat Shinji

Halmashauri ya Mji Kasulu mkoani Kigoma, imejipanga kutekeleza uzinduzi wa miradi mbalimbali ya Serikali katika kampeni ya Mbio za Mwenge wa Kitaifa zinazotarajiwa kuanza itakapofika Septemba mwaka huu.

Akizungumza na Buha Fm Radio leo Baada Kikao cha maandalizi ya Mbio za Mwenge Mratibu wa zoezi hilo Ndg. Daudi Stinga amesema halmashauri ya Mji Kasulu imejipanga kufanya vizuri katika zoezi hilo ili kuendelea kushika nafasi ya kwanza kama ilivyokuwa mwaka 2024.

Sauti ya mratibu wa Mbio za mwenge halmashauri ya mji kasulu Ndg. Daudi Stinga.
Pichani ni wajumbe wa mkutano wa maandalizi ya Mbio za Mwenge katika halmashauri ya Mji Kasulu. Picha na Sharifat Shinji.

Aidha Stinga amesema mwaka huu watazindua miradi mbalimbali ikiwemo miradi ya Afya, Elimu, Barabara, maji Pamoja na miradi ya mapato ya ndani huku akiwaomba wadau kuonga mkono jitihada za serikali katika kutekeleza miradi katika kukuza Uchumi wa nchi.

Sauti ya Daudi Stinga mratibu wa mbio za Mwenge.

Katika hatua nyingine Mwl. Zawadi Mnana ambaye ni mjumbe wa Mbio za Mwenge 2025 amesema  mwaka huu wameanza mapema kujiandaa ili kubakia katika nafasi ya kwanza na nafasi za juu zaidi kitaifa.

Sauti ya Mwl. Zawadi Mnana Mjumbe wa kikao cha maandalizi ya mbio za Mwenge mwaka 2025.

Kwa upande wake Mwl. Michael Benezeth ambaye ni Mwenyekiti wawakuu wa shule katika halmashauri ya Mji Kasulu amesema maandalizi yameanza mapema ili wajumbe wapate kupendekeza maeneo ambayo yanauhitaji ya kufikiwa na Mwenge wa kitaifa.

Sauti ya Mwl. Mwl. Michael Benezeth mjumbe na mdau wa maandalizi ya mbio za mwenge mwaka 2025.

Halmashauri ya Mji Kasulu kwa mwaka 2024 katika zoezi la mbio za mwenge ilishika nafasi ya kwanza kati ya halmashauri nane za mkoa wa Kigoma na kushika nafasi ya 46 kitaifa hivyo mwaka huu wadau wa maendeleo ya mbio za Mwenge wamejipanga kushika nafasi za juu zaidi kitaifa ili kuipa hadhi halimashauri na mkoa kwa ujumla.

Pichani ni wajumbe na wadau wa mbio za mwenge wakiwa katika kikao cha maandalizi kuelekea zoezi la kukimbiza mwenge mwezi Septemba katika halmashauri ya mji Kasulu. Picha na Sharifat Shinji.