Buha FM Radio

Uzazi wa mpango watajwa kuleta furaha katika familia

May 19, 2025, 7:37 pm

Chati ya uzazi wa mpango kwa mzunguko wa mwezi mzima. Picha na (James Herbal Clinic)

Jamii yashauriwa kufuata na kutumia njia za uzazi wa mpango ili kupunguza utapiamlo unaoweza kujitokeza kutokana na familia nyingi kujifungua bila kufuata njia za uzazi wa mpango.

Na: Kudra Mbali

Wananchi katika halmashauri ya Mji Kasulu wameshauriwa kufuata na kutumia njia za uzazi wa mpango ili kuondokana na madhara ambayo yanaweza kujitokeza kutokana na kujifungua bila mpangilio hali ambayo inaweza kupelekea wazazi kushindwa kutunza na kulea familia zao.

Akizungumza na Buha FM radio muuguzi kutoka zahanati ya Nyumbigwa katika Halmashauri ya Mji Kasulu Bi. Beatrice Machibya Mei 19 mwaka huu na kubainisha athari ambazo mzazi anaweza kuzipata kutokana na kuendelea kujifungua bila kufata mpangilio wa uzazi.

Sauti ya muuguzi Bi. Beatrice Machibya akieleza jinsi uzazi wa mpango ulivyo leta changamoto za maisha katika jamii.

Aidha Bi. Machibya amesema uzazi wa mpango ukifuatwa kwa usahihi utaleta faraja katika familia kwani huwawezesha wanafamilia kuwa na muda wa kutosha katika kufanya kazi za maendeleo kuliko wale wanaoishi bila kufuata mpangilio wa uzazi.

Sauti ya muuguzi Bi. Beatrice Machibya akieleza jinsi uzazi wa mpango ulivyo na faida katika jamii.

Kwa upande wao baadhi ya wakazi katika Halmashauri ya Mji Kasulu wameeleza namna wanavyoelewa kuhusu mpango wa uzazi katika familia huku wengine wakitaja faida za kufuata mpangilio wa uzazi katika ndoa na familia.

Sauti za wananchi wakieleza jinsi wanavyoelewa kuhusu mpango wa uzazi na faida zake.

Kwa muuji wa shirika la takwimu Tanzania NBC mwaka 2022 lilichapisha takwimua zinazoonesha asilimia 38 ya wanawake walioolewa wanatumia njia yoyote ya uzazi wa mpango, ikijumuisha asilimia 31 ya wanaotumia njia zozote za kisasa na asilimia 7 ya wanawake wanaotumia njia za asili za uzazi wa mpango.

Chati ya uzazi wa mpango kwa mzunguko wa mwezi mzima. Picha na (James Herbal Clinic)