Buha FM Radio

Kasulu kupendezeshwa na lami kila kona

May 17, 2025, 8:33 pm

Picha ni barabara ya lami ambazo zitajengwa kila mtaa katika halmashauri ya Mji Kasulu. Picha na Mbaraka Shabani.

Serikali katika Halmashauri ya Mji kasulu mkoani Kigoma imeahidi kutekeleza ujenzi wa miundombinu ya barabara za mitaa kwa kiwango cha lami ili kulahisisha shughulii za usafirishaji zinazofanyika katika Mji huo.

Na: Mbaraka Shabani

Halmashauri ya Mji kasulu mkoani Kigoma imepanga kutengeza na kuboresha barabara za mitaa katika kata zote zilizopo ndani ya halimashauri hiyo kwa kiwango cha lami ili kulahisisha shughuli za usafirishaji.

Hayo yamebainishwa na mwenyekiti wa halmasauri ya mji Kasulu Bw.Norah Noel wakati akizungumza na Buha Fm radio juu ya mchakato wa zoezi la kurekebisha barabara hizo pamoja na miradi mingine inayoendelea kutekelezwa na serikali wilayani humo.

Sauti ya mwenyekiti wa halmasauri ya mji Kasulu Bw.Norah Noel akielezea kuhusu barabara na utekelezaji utakavyofanyika.
Pichani ni muonekano wa baadhi ya barabara za mitaa katika halmashauri ya mji Kasulu mkoani kigoma. Picha na Mbaraka Shabani.

Aidha Noel ameongeza kwa kusema baadhi ya barabara zitajengwa na serikali huku nyingine kutekelezwa na shirika la maendeleo la kimataifa UNDP hali ambayo itaufanya mji wa kasulu kufunguka kibiashara kitu ambacho amewasa wakazi wa mji huo kuchangamkia fursa za ajira zitakazokuwa sinatolewa na wakandarasi wa shughuli hiyo ya ujenzi.

Sauti ya mwenyekiti wa halmasauri ya mji Kasulu Bw.Norah Noel akielezea kuhusu barabara na utekelezaji utakavyofanyika na kutaja fursa kwa wakazi wa eneo husika.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi Mwl.Dismas Mbee Msafu amepongeza juhudi za serikali kuendelea kuboresha miundombinu ya Barabara huku akiwataka TARURA kutengeneza mifereji ya maji ili kuepuka ufalibifu unaojitokeza kila inaponyesha mvua na maji kuelekea barabarani.

Sauti ya mwananchi Mwl.Dismas Mbee Msafu akieleza ukosefu wa mifereji ya maji katika barabara za mitaa.

Halmashauri ya Mji Kasulu Barabara nyibgi za mtaa zinakabiliwa na mashimo yaliyosababishwa na mvua za msimu hivyo serikali imedhamilia kutekeleza ujenzi wa Barabara katika maeneo yote ya Mji huo lengo nikuboresha sekta ya usafirishaji na kuupa hadhi mji wa Kasulu  na kuweka katika mpangilio bora wa kuvutia.

Muonekano wa barabara ya iliyojengwa kwa kiwango cha lami katika Halmashauri ya mji kasulu.Picha na Mbaraka Shabani.