Buha FM Radio

Mikopo ya halmashauri ya 10% irejeshwe kwa wakati

April 27, 2025, 1:34 pm

Mbunge wa Jimbo la Kasulu mjini Prof. Ndalichako akikabidhi hundi ya fedha za mikopo ya 10% kwa vikundi.

“Niwasihi mnavyofurahi kukopa fedha hizi na kurejesha iwe hivyo ili kupata nafasi ya kukopa zaidi kwa sababu kunabaadhi ya vikundi vilikopa awamu iliyopita ilishindwa kurejesha kutokana na kutokuwa na matumizi sahihi ya fedha hizo”

Na Paulina Majaliwa

Mbunge wa jimbo la Kasulu Mjini Prof. Joyce Ndalichako amewaomba wanufaka wa mikopo ya serikali ya asilimia kumi  ya mapato ya ndani kutumia kwa usahihi pesa hizo ili kuweza kuendesha miradi waliyoanzisha na kurejesha mikopo kwa wakati ili kuwapa nafasi wananchi wengine kukopa  fedha hizo.

Amesema hayo April 26,2025 wakati akikabidhi hundi ya mikopo hiyo na vifaa kwa vikundi  mbalimbali  katika viwanja vya Halmashauri Mji Kasulu na  kusema kuwa baadhi ya vikundi  vimekuwa  vikishindwa  kurejesha  pesa  hizo  kutokana na kutoendeleza  miradi waliyoanzisha wakati wa kukopa mikopo hiyo.

Sauti ni Mbunge Prof. Ndalichako

Aidha amesema vikundi ambavyo havijapata mkopo  huo ni kwa sababu havijakidhi vigezo hivyo waendelee kuboresha taarifa zao ili wapate mikopo  kwa awamu nyingine kwani mikopo hii ni ya mwendelezo pia wafikishe taarifa zao kwa mkurugenzi wa halimashauri Mji Kasulu ili taarifa zao zitambulike.

Sauti ni Mbunge Prof. Ndalichako 2.

Kwa upande wao baadhi ya wanufaika wa mikopo hiyo wilayani Kasulu wameishukuru serikali  kwa kuwapatia mikopo hiyo kwani itawasaidia katika kuendeleza miradi mbalimbali kama vile biashara,kilimo na ufugaji pamoja na kuinua uchumi wao binafsi kutokana na elimu waliyoipata na kuahidi kuwa watafanya kazi kwa bidii ili kujikwamua kiuchumi.

Sauti ya za wanufaika wa mikopo.

 Mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halimashauri nchini Tanzania ni sehemu ya juhudi za serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania kuhamasisha maendeleo ya kiuchumi kwa makundi maalum ikiwa ni pamoja na wanawake,vijana na watu wenye ulemevu na fedha  hizi  hutolewa kwa vikundi vilivyosajiliwa ambapo katika Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu kwa awamu hii imetenga bajeti ya kiasi cha shilingi milioni 514 ambapo imetoa  mikopo yenye thamani ya  kiasi cha shilingi milioni 433 kwa vikundi 32 vyenye jumla ya wanufaika 230 waliokizi vigezo vya kupokea mikopo hiyo.

Baadhi ya wanufaika wa mikopo ya asilimia 10 katikaHalmashauri ya Mji Kasulu.