Kagera Community Radio

DC Siima aagiza usafi kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi

September 1, 2025, 6:23 pm

Mkuu wa wilaya ya Bukoba Erasto Siima

Wananchi na wamiliki wa maduka wilayani Bukoba mkoani Kagera wametakiwa  kufanya usafi wa jumla kila jumamosi ya mwisho wa mwezi ili kuepukana na magonjwa ya mlipuko kama kipindupindu na kutunza taswira nzuri ya wilaya hiyo.

Na Avitus Kyaruzi

Mkuu wa wilaya ya Bukoba, mkoani Kagera Erasto Sima, amewataka wananchi na wamiliki wa maduka wilayani humo kufanya usafi wa jumla kila jumamosi ya mwisho wa mwezi ili kuepukana na magonjwa na kuuweka mji katika hali ya usafi.

Baadhi ya wananchi wa wilaya ya Bukoba wakifanya usafi

DC.Siima amesema hayo alipo ambatana na mkurugenzi wa halmashauri ya manispaa ya Bukoba Ndg. Jacob S. Nkwera na kamati ya usalama ya wilaya na kuungana na wananchi wa kata ya Bilele manispaa ya Bukoba, katika zoezi la kufanya usafi wa mazingira, ikiwa ni sehemu ya utaratibu wa usafi wa jumamosi ya mwisho wa kila mwezi.

Mhe. Sima amewataka wananchi kuendeleza mshikamano na ushirikiano katika kuhakikisha mji wa Bukoba unakuwa safi na salama kwa afya ya jamiiĀ  na kwamba usafi wa mazingira ni wajibu wa kila mmoja na ni msingi wa kujikinga na magonjwa ya milipuko.

Kulia ni mkuu wa wilaya ya Bukoba Erasto Siima akishiriki katika zoezi la kufanya usafi

Katika hatua nyingine mkuu huyo wa wilaya ya Bukoba amewataka wakala wa barabara mjini na vijiji TARURA, na wakala wa barabara nchini TANROADS kuhakikisha wanaifanyia usafi mitaro ya kupitisha maji iyopo pembezoni mwa barabara ambayo imefunikwa.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Bukoba Erasto Siima

Nao baadhi ya wananchi walioshiriki zoezi hilo wamepongeza uongozi wa wilaya na Halmashauri kwa kuungana nao bega kwa bega na kuonesha mfano wa vitendo katika masuala ya kijamii.

Baadhi ya wananchi wa kata ya Bilele wakifanya usafi