Kagera Community Radio

Waendesha pikipiki Biharamulo watakiwa kufuata sheria

June 21, 2025, 5:12 pm

Baadhi ya waendesha pikipiki (bodaboda) walioshiriki kikao cha usalama barabarani

Waendesha pikipiki (maarufu bodaboda) wilayani Biharamulo mkoani Kagera wamesisitizwa juu ya kufuata sharia za usalama barabarani ikiwemo uvaaji wa kofia ngumu ili kulinda usalama wao na abilia na kuepukana na faini wawapo barabarani.

Na.Anold Deogratias

Waendesha pikipiki (maarufu bodaboda) wilayani Biharamulo mkoani Kagera wametakiwa kufuata sheria na kanuni za usalama barabarani ili kuepukana na ajali zinazoweza kuzuhirika pamoja na kuepuka faini.

Wito huo umetolewa na mkuu wa kitengo cha usalama barabarani wilaya ya Biharamulo, Bw.Enock Chengula, wakati akizungumza kwenye kikao cha waendesha pikipiki (maarufu bodaboda) kilichoitishwa na mabalozi wa usalama wa barabarani mkoa wa Kagera, kilichofanyika wilayani Biharamulo.

Mkuu wa kitengo cha usalama barabarani wilaya ya Biharamulo Enock Chengula

Bw. Chengula amewataka waendesha pikipiki hao kufuata sheria za uasalama barabarani ikiwemo uvaaji wa kofia ngumu (helmet) ili kujikinga na ajali lakini pia amewasisitiza juu ya kuwa na utambulisho wa maeneo wanapofanyia kazi.

  Sauti ya Enock Chengula, mkuu wa usalama barabarani wilaya ya Biharamulo

Kwa upande wake mwenyekiti wa mabalozi wa usalama barabarani mkoa wa Kagera (RSA) Mohamed Ramadhan Makonda amewataka waendesha pikipiki hao kuvaa nguo zinazoonyesha utambulisho wao pamoja na zenye rangi maalum ili kuwasaidia kuonekana vizuri hasa nyakati za usiku.

 Sauti ya Ramadhan Makonda, balozi wa usalama barabarani

Nao baadhi ya waendesha pikipiki wilayani Biharamulo Adinan Majdi na Allen Agustin wamesema kuwa kuna umuhimu wa uvaaji wa kofia ngumu (helmet) kwao na kwa abilia ili kulinda usalama wao.

  Sauti ya waendesha pikipiki
Waendesha pikipiki walioshiriki kikao cha usalama barabarani Biharamulo