Kagera Community Radio

Hedhi bila vikwazo shuleni

April 24, 2025, 10:10 am

Wanafunzi wa shule ya sekondari Nyanga manispaa ya Bukoba wakifurahia taulo za kike kutoka shirika la Agri-thaman. Picha na Fabius Clavery

Ukosefu wa taulo za kike kwa wanafunzi ni miongoni mwa sababu zinazowafanya wanafunzi kushindwa kuudhuria masomo katika kipindi cha hedhi

Na Fabius Clavery

Hedhi salama ni haki ya msingi kwa kila mwanafunzi wa kike. Kupitia elimu sahihi, upatikanaji wa vifaa salama vya kujisitiri, na kuondoa unyanyapaa, ili kuwasaidia wasichana kushiriki kikamilifu katika masomo yao bila vikwazo. Mpango huu unalenga kuongeza uelewa, kuboresha mazingira ya shule, na kuwawezesha wanafunzi wa kike kujivunia mabadiliko ya miili yao kwa heshima na usalama.