Bunda FM Radio
Bunda FM Radio
January 13, 2026, 7:30 pm

”Hata kama mwanafunzi hajakamilisha mahitaji yake ya shule kama vile sare za shule apokelewe asajiliwe na aendelee na masomo mwalimu mkuu atake mzuia mwanafunzi atachukuliwa hatua za kisheria ikiwemo kupokonywa ukuu wa shule” Mkuu wa wilaya ya Bunda Aswege Enock Kaminyoge
Na Amos Marwa
Mkuu wa wilaya ya Bunda Aswege Enock Kaminyoge amewataka walimu wakuu wa shule za misingi na sekondari kuwapokea wanafunzi bila masharti yoyote hatakama hawajakamilisha mahitaji yote ya shule.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Kaminyoge amesema kuwa walimu wanao wajibu wa kuwapokea wanafuzi wote kuanza darasa wali, la kwanza na kidato cha kwanza hatakama hawajakamilisha mahitaji ya shule ikiwemo sare za shule na kuongeza kuwa mwalimu mkuu atakae shindwa kufuata maagizo hayo atachukuliwa hatua za kisheria
Ametoa wito kwa wazazi na walezi kuwapeleka watoto wote watoto yenye shule ili kuanza muhula mpya wa masomo ulionza leo januari 13, 2026.
Aidha, amewataka wenyeviti wa mitaa na vitongoji kuhakikisha kwenye maeneo yao wanafunzi wanaopaswa kwenda shule wanaenda kwa wakati .
Muhula mpya wa masomo umeanza leo januari 13, 2026 na ikiwa malengo ya serikali ni kuwa ifikapo januari 30, 2026 wanafunzi wote wameripoti shuleni kwa ajili ya kwendelea na masomo yao.
