Bunda FM Radio

Serikali yajipanga kupunguza upotevu wa maji Bunda

January 7, 2026, 7:44 pm

Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Kundo Andrea Mathew akizungumza na wananchi pamoja na watumishi wa Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira Bunda (BUWWSA), alipokuwa mgeni rasmi katika hafla ya ya kuweka jiwe la Msingi mradi wa Uboreshaji wa Mtandao wa Bomba Kutoka Migungani hadi Kaswaka. picha na Amos Marwa

Kuna sababu nyingi za upotevu wa maji ikiwemo miundombinu kuwa chakavu, uchepushaji wa maji mita zinazotumika kwa sasa na matumizi yasiyozingatia mahitaji halisi” Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Kundo Andrea Mathew

Na Amos Marwa

Serikali imejipanga kupunguza tatizo la upotevu wa maji kwa kuweka miundombinu imara inayoendanda na nguvu ya maji ikiwemo kutoa bomba za plastiki na kuweka bomba za chuma ili kuwahakikishia wananchi huduma hiyo  muda wote.

Hayo yamebainishwa na Naibu waziri wa maji Mhandisi Kundo Andrea Mathew aliyekuwa mgeni rasmi katika hafla ya kuweka jiwe la msingi mradi wa Uboreshaji wa Mtandao wa Bomba Kutoka Migungani hadi Kaswaka iliyofanyika eneo la Mtaa wa Migungani mjini Bunda.

Sauti ya Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Kundo Andrea Mathew akibainishia njia za kuzuia upotevu wa maji.

Kundo amewataka wananchi kuwa wazalendo na kulinda miundombinu ya maji na kutoa taarifa kwa jeshi la polisi wanapobaini mtu yeyote anaehusika na uharibifu huo.

Sauti ya Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Kundo Andrea Mathew akiwaasa wananchi kulinda miundombinu ya Maji
Watumishi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Bunda (BUWASSA) wakitoa burudani ya nyimbo katika hafla ya kuweka jiwe la Msingi mradi wa Uboreshaji wa Mtandao wa Bomba Kutoka Migungani hadi Kaswaka iliyoongozwa na Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Kundo Andrew Mathew eneo la Mtaa wa Migungani mjini Bunda. Picha na Amos Marwa

Nae  Mkurugenzi wa Mamlaka ya maji safi na Usafi wa Mazingira Bunda (BUWSSA) Esther Gilyoma amesema Mamlaka inapoteza zaidi ya milioni 600 kama mapato ya upotevu wa maji kwa mwaka.

Sauti Mkurugenzi wa Mamlaka ya maji safi na Usafi wa Mazingira Bunda (BUWSSA) Esther Gilyoma akielezea athari za upotevu wa maji

Kwa upande wake mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini  Ester Amos Bulaya amemshukuru Naibu waziri wa maji kwa kukagua miradi ya maji jimbo la Bunda mji na kusema kuwa kukamilika kwa mradi huo kutasaidia kupunguza upotevu wa maji na kumtua ndoo mama kichwani.

Sauti ya Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini  Ester Amos Bulaya akitoa shukrani kwa Naibu waziri wa Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Kundo Andrea Mathew
Sehemu ya wananchi waliofika kushuhudia uwekaji wa jiwe la Msingi mradi wa Uboreshaji wa Mtandao wa Bomba Kutoka Migungani hadi Kaswaka iliyoongozwa na Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Kundo Andrew Mathew eneo la Mtaa wa Migungani mjini Bunda. picha na Amos Marwa