Bunda FM Radio

Mitaji changamoto kwa vyama vya ushirika na mikopo(SACCOS)

November 28, 2025, 7:38 pm

Shukrani Modest Mihungo Afisa ushirika Bunda mji akizungumza na wanachama wa chama cha ushirika wa akiba na mikopo cha Kibara biashara (SACCOS) wakati wa Mkutano mkuu wa chama hicho uliofanyika novemba 28. Picha na Amos Marwa

Nashauri kamati ya mikopo kujua historia za wakopaji hasa kwa wakopaji wageni ili kuepuka wakopaji kutokomea na fedha za chama”Shukrani Modest Mihungo Afisa ushrika Bunda mji

Na Amos Marwa

Wanachama wa chama cha ushirika wa akiba na mikopo cha Kibara biashara (SACCOS) wametakiwa kujiwekea akiba na hisa kwa wingi ili kupunguza tatizo la upungufu wa mitaji katika chama chicho.

Hayo yamebainishwa na Shukrani Modest Mihungo afisa wa vyama vya ushirika Bunda mji alie kuwa mgeni rasmi katika mkutano wa mwaka wa chama hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Bunda fm radio na kusema kuwa kila mwanachama anatakiwa kuwa na utamaduni wa kujiwekea akiba na hisa mara kwa mara ili kukuza chama hicho na kupunguza tatizo hilo la upungufu wa mitaji.

sauti ya Shukrani Modest Mihungo afisa wa vyama vya ushirika Bunda mji akiwataka wanachama kujiwekea akiba na mikopo kulinda uhai wa chama hicho.
Washiriki wa mkutano mkuu wa 18 wa chama cha ushirika wa akiba na mikopo cha Kibara biashara (SACCOS) wakifuatilia mkutano huo kwa umakini. Picha na Amos Marwa

Awali akisoma taarifa ya chama hicho wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu makamu mwenyekiti Hamadi Nyamanda amesema kuwa SACCOS hiyo inakabiliwa na chamangamoto lukuki lakini upungufu wa mitaji ndio kikwazo kikubwa cha maendeleo katika SACCOS hiyo

Sauti ya makamu mwenyekiti wa chama cha ushirika wa akiba na mikopo cha Kibara biashara (SACCOS) Hamadi Nyamanda akisoma taarifa mbele ya mgeni rasmi na kuibua changamoto ya mitaji

Kwa upande wao wanachama walioshiriki mkutano huo wamesema chama hicho kimekua faida kubwa kwao na kuahidi kuwa wataongeza hisa na kukopa kwa wingi ili kupunguza tatizo la uhaba wa mitaji

Sauti za wanachama waliohudhuria mkutano mkuu wakielezea faida walizopata katika chama hicho na mikakati yao kwa mwaka ujao wa 2026

Mzee Barton Baraga mmoja wa wanachama wa chama cha chama cha ushirika wa akiba na mikopo cha Kibara biashara (SACCOS) akichangia hoja katika mkutano mkuu wa chama hicho. Picha na Amos Marwa

Mkutano huo wa 18 wa chama cha ushirika wa akiba na mikopo cha Kibara biashara (SACCOS) umeazimia kuwashirikisha wadau mbalimbali wa maendeleo kushirikiana na chama hicho huku kamati za ukopeshaji zikiweka mikakati kwa wakopaji wasio lipa kwa wakati kwa kuwafikisha katika vyombo vya sheria.