Bunda FM Radio

Wakulima Mara kunufaika na mbegu za ruzuku

November 13, 2025, 5:33 pm

Benard Mathew afisa kilimo kata ya Bunda stoo aliekuwa mgeni rasmi kwa niaba ya Afisa kilimo wiliya ya Bunda kwenye mkutano wa mtandao wa vikundi vya wakulima Tanzania (MVIWATA) mkoa wa Mara akizungumza na vikundi mbalimbali vya wakulima. picha na Amos Marwa

Nawaomba wakulima wote kujiunga kwenye mtandao wa vikundi vya wakulima Tanzania (MVIWATA) ili waweze kuwa na sifa za kukopeshwa pembejeo za kilimo” Benard Mathew afisa kilimo kata ya Bunda stoo

Na Amos Marwa

Wakulima wadogowagogo mkoa wa Mara wamehakikishiwa fursa za masoko na upatikanaji wa mbegu za ruzuku ili kuimarisha maslahi yao. Hayo yamebainishwa na Benard Mathew afisa kilimo kata ya Bunda stoo aliekuwa mgeni rasmi kwa niaba ya Afisa kilimo wilaya ya Bunda kwenye mkutano wa mtandao wa vikundi vya wakulima Tanzania (MVIWATA) Kwa mkoa wa Mara uliofanyika ukumbi wa vileji wilaya ya Bunda  na kusema kuwa serikali kupitia wizara ya kilimo itatoa mbegu za ruzuku, viwatilifu na masoko ya uhakika ili kuleta tija kwa wakulima.

Hayo yamebainishwa na Benard Mathew afisa kilimo kata ya Bunda stoo aliekuwa mgeni rasmi kwa niaba ya Afisa kilimo wilaya ya Bunda kwenye mkutano wa mtandao wa vikundi vya wakulima Tanzania (MVIWATA) Kwa mkoa wa Mara uliofanyika ukumbi wa vileji wilaya ya Bunda  na kusema kuwa serikali kupitia wizara ya kilimo imetoa mbegu za ruzuku, viwatilifu na masoko ya uhakika ili kuleta tija kwa wakulima

Sauti ya Benard Mathew afisa kilimo kata ya Bunda stoo akizungumza na wakulima mkoa wa Mara

Akisoma taarifa katibu wa  MVIWATA mkoa wa Mara Baraka Sagare amesema lengo la chombo hicho ni kuwezesha mawasiliano miongoni mwa wakulima wadogo wadogo  ili kujenga ushawishi na utetezi kwa manufaa ya wakulima hao

Sauti ya katibu wa  MVIWATA mkoa wa Mara Baraka Sagare akielezea malengo ya MVIWATA kwa wakulima mbele ya mgeni rasmi na wakulima.

Mtandao wa vikundi vya wakulima Tanzania(MVIWATA) umeanzishwa kwaka 1993 ikiwa ni chombo kinachowaunganisha wakulima wadogowadogo na kutengeneza sauti moja.

Baadhi ya wakulima mkoa wa mara wakiwa kwenye kikao cha mtandao wa vikundi vya wakulima Tanzania (MVIWATA) kilichofanyika ukumbi wa Vileji wilaya ya Bunda. Picha na Amos Marwa