Bunda FM Radio
Bunda FM Radio
October 16, 2025, 12:37 pm

”Nchi yoyote ili iwe na maendeleo ni lazima kuwepo na amanai na utulivu hivyo kila mtu anawajibu wa kulinda tunu hii ya amani”Mkuu wa polisi wilaya ya Butiama(OCD)rakibu mwandamizi wa polisi Daudi Methew Ibrahim
Na Amos Marwa
Wananchi mkoa wa Mara wahimizwa kulinda na kuimarisha amani utulivu na usalama katika kipindi cha uchaguzi na baada ya uchaguzi mkuu.
Hayo yamebainishwa na Mkuu wa polisi wilaya ya Butiama(OCD) Mrakibu Mwandamizi wa jeshi la polisi Daudi Methew Ibrahim wakati akizungumza na Bunda FM katika kipindi cha Busati la Habari na kusema kuwa tunapaswa kukumbatia amani tuliyonayo ili twendelee kulijenga taifa letu kiuchumi na kuongeza kuwa kama amani itavurugwa watu hawatapata nafasi ya kujihusisha na uzalishaji mali badala yake watakuwa wakikimbia machafuko.