Bunda FM Radio

Upungufu wa walimu changamoto kwa shule za sekondari Bunda Mji

October 3, 2025, 3:16 pm

Sehemu ya wahitimu wa kidato Cha nne kwenye mahafari ya Pili ya Bunda stoo sekondari 2025. Picha na Amos Marwa

”Shule yetu inakabiliwa na uhaba wa Walimu na upungufu wa Maabara jambo linalofanya tushindwe kujifunza masomo yetu kwa ufanisi” maneno ambayo ni sehemu ya risala kidato cha nne Bunda stoo Sekondari.

Na Amos Marwa

Wadau mbambali wa elimu wametakiwa kushirikiana ili kuondoa changamoto ya upungufu wa Walimu  uliopo katika shule ya sekondari Bunda stoo na shule zingine zilizopo halmashauri ya mji wa Bunda.

Rai hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Mtaa wa Idara ya maji  Mtaki Bwire aliekuwa mgeni rasmi katika hafla ya mahafari ya pili ya kidato cha nne katika shule ya sekondari Bunda stoo yaliyofanyika katika viwanja vya shule hiyo na kuwaomba Afisa elimu kata na Afisa elimu sekondari kuwasilisha uhitaji wa walimu kwa mkurugenzi wa Mji wa Bunda ili kuondoa changamoto hiyo ikiwa ni sehemu ya kujibu risala iliyosomwa na wa hitimu wa shule hiyo.

Sauti ya Mgeni rasmi Mtaki Bwire akiwataka Wadau mbambali wa elimu kushirikiana ili kuondoa changamoto ya upungufu wa Walimu  uliopo katika shule ya sekondari Bunda stoo .
Mgeni rasmi Mtaki Bwire akitoa hotuba yake kwenye mahafari ya Pili ya kidato Cha nne Bunda stoo sekondari ikiwa ni sehemu ya kujibu risala iliyosomwa na wahitimu wa shule hiyo. Picha na Amos Marwa.

Kwa upande wa Mwalikishi wa wazazi wa wahitimu Noella Richard amewashukuru Walimu kwa kuwalea watoto wao kwa madili mema kwa miaka minne na kuwataka wahitimu hao kutumia maadili  hayo katika jamii.

Sauti ya Mwalikishi wa wazazi wa wahitimu Noella Richard akitoa shukrani kwa Walimu kwa kuwalea watoto wao kwa madili mema kwa miaka minne
Wahitimu wa kidato Cha nne wakionyesha umahiri wao kwa vitendo kwa Yale waliojifunza madarasani mbele ya Mgeni rasmi na wazazi waliohidhuria mahafari hiyo. Picha na Amos Marwa

Nao wahitimu wa mahafari hayo wamewashukuru walimu kwa ushirikiano wao katika safari ya miaka mi nne na kuahidi kuwa watafanya vizuri katika mitihani yao itakayofanyika novemba mwaka huu.

Sauti za wahitimu wakitoa shukrani zao kwa Walimu kwa ushirikiano wa pamoja kwa miaka minne na kuelezea maandalizi yao kwelekea mitihani yao ya kidato cha nne itakayofanyika novemba mwaka huu.

 Sehemu ya Wazazi waliohidhuria hafla ya Mahafari ya Pili  kidato Cha nne Bunda stoo Sekondari 2025. Picha na Amos Marwa

Jumla ya wahitimu 333 katika shule ya sekondari Bunda stoo wanatarajia kuingia katika mitihani ya kidato cha nne 2025  ikiwa wavulana ni 178 na wasichana 155 .