Bunda FM Radio

Mara wajiandaa kupokea mwenge wa uhuru

August 13, 2025, 6:04 pm

Mkuu wa mkoa wa Mara Kanali Evans Alfred Mtambi akizungumza na wandishi wa habari kuhusu mapokezi ya mwenge wa uhuru mkoa wa Mara . Picha na mtandao

Tukumbuke kuwa mwenge wa uhuru huleta tumaini pasipo tumaini, upendo palipo na chuki ”Mkuu wa mkoa wa Mara Kanali Evans Alfred Mtambi.

Na Amos Marwa

MKuu wa mkoa wa Mara  Kanali Evans Alfred Mtambi amewataka wananchi na wadau wote kujitokeza kwa wingi kushiriki mbio za mwenge wa uhuru kwa kipindi chote mwenge utakapo kuwa mkoa wa Mara.

Akizungumza na wandishi wa habari Mtambi amesema kuwa mkoa wa Mara utapokea mwenge wa uhuru kutoka mkoa wa Simiyu agosti 15, 2025 na mapokezi hayo yatafanyika katika uwanja wa shule ya msingi Balili.

Sauti ya Mkuu wa mkoa wa Mara Kanali   Evans Alfred Mtambiakwataka wananchi na wadau wote kujitokeza kupokea mwenge wa uhuru.

Ameongeza kuwa agosti 15 mwenge wa uhuru utaanza kukimbizwa  katika Halmashauri ya mji wa Bunda na kupitia Halmashauri zote 9 za mkoa Mara na kuhitimisha mbio hizo agosti 23 katika Halmashauri ya wilaya ya Bunda.

Sauti ya Mkuu wa mkoa wa Mara Kanali  Evans Alfred Mtambi akitoa ratiba ya mwenge wa uhuru katika halmashauri zote za mkoa wa Mara

Mwenge wa uhuru ukiwa Mkoa wa Mara utakimbizwa jumla ya kilometa  1,123  ukitembelea , kukagua, kuweka mawe ya Msingi, kufungua na kuzindua jumla ya miradi 68  ya maendeleo yenye thamani ya jumla shilingi bilioni 26.54.