Bunda FM Radio

Janeth Moters yashika mkono kanisa la AICT Changuge

August 10, 2025, 8:22 pm

Mkurugenzi wa kampuni ya Janeth Moters Janeth Webiro baada ya hafla ya changizo iliyofanyika katika kanisa la AICT Changuge. Picha na Amos Marwa

Mimi Janeth naamini katika kutoa katika mizunguko yangu yote naamini ukimtolea Bwana unabarikiwa zaidi tujifunze kutoa kwa moyo tuone baraka za Bwana zinavomiminika”Mkurugenzi wa kampuni ya Janeth Moters Janeth Webiro

Na Amos Marwa

Kampuni ya Janeth Motors limited inayojishughulisha na uuzaji wa magari, pikipiki, upimaji na uzaji wa viwanja imetoa vifaa vya Mziki Maiki 5 na kiasi cha pesa za kitanzania Laki Tatu  katika kanisa la AICT Changuge kwenye  hafla ya Changizo iliyofanyika katika kanisa hilo ikiwa ni sehemu ya  kurudisha kwa jamii.

Akizungumza katika hafla hiyo Mkurugenzi wa kampuni hiyo Janeth  Webiro aliekuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo amesema kumtolea Mungu ni sehemu ya Baraka na mafanikio.

Sauti ya Mkurugenzi wa kampuni ya Janeth Moters Janeth Webiro akizungumza na waumini wa kanisa la AICT Changuge kwenye hafla ya changizo iliyofanyika katika kanisa hilo.
Meneja wa Kampuni ya Janeth Moters Waiter Natay akizungumza na na waumini wa kanisa la AICT Changuge kwenye hafla ya changizo iliyofanyika katika kanisa hilo. Picha na Amos Marwa

Meneja wa Kampuni ya hiyo Waiter Natay amesema biashara na imani vinaendana hivyo kampuni hiyo  imejitolea kushirikiana na  jamii  kwa ajili ya maendeleo.

Sauti ya Meneja wa Kampuni ya Janeth Moters Waiter Natay akielezea uhusiano uliopo kati ya biashara na imani.

Kwa upande wao viongozi wa kanisa la AICT Changuge  wamesema vifaa hivyo vitasaidia kanisa hilo kueneza injili na kuishukuru kampuni ya Janeth Motors na  kuwataka kuwa na moyo wa kwendelea kusaidia jamii.

Sauti ya viongozi wa kanisa la AICT Changuge wakitoa neno la shukrani kwa kampuni ya Janeth Moters baada ya kumalizika hafla ya changizo.

Hafla hiyo ya Changizo  imeandaliwa na idara ya wanawake Makanisa ya AICT Changuge, Kisangwa, Mirungu na Bukore kutoka kata ya Mcharo kwa ajili ya kupata michango ya kweneza utume na kuendeleza kanisa hilo.

Baadhi ya waumini wa kanisa la AICT changuge wakiendesha zoezi la changizo lililofanyika katika kanisa hilo. Picha na Amos Marwa