Bunda FM Radio

Wanawake, vijana, wenye ulemavu Bunda mji wapewa mikopo

July 26, 2025, 10:13 am

Katibu tawala wilaya ya Bunda Salmu Alfan Mtelela akikabidhi hundi ya shilingi milioni mianne thelathini na tano ikiwa ni sehemu ya mkopo kwa vikundi vya akina Mama, Vijana na wenye ulimaavu. Picha na Amos Marwa

Mkatumie mikopo hii kwa lengo lilopangwa ili muweze kurejesha kwa wakati ili vikundi vingine vikanufaike na mikopo hii hatutegemie kuwaona katika kumbi za staarehe kama baa mkinywa bia kutumia fedhaa hizi za mikopo” Katibu tawala Wilaya ya Bunda Salmu Alfan Mtelela

Na Amos Marwa

Vikundi vya akina mama, Vijana na wenye ulemavu wilaya ya Bunda wametakiwa kutumia fedha za mikopo inayotolewa na Halmashauri kwa lengo lilokusudiwa  ili kusaidia vikundi hivyo kuondokana na hali ya umasikini.

Hayo yamebainishwa na Katibu tawala Wilaya Bunda Salmu Khalfan Mtelela aliekuwa  mgeni rasmi wakati wa hafla ya kukabidhi Hundi ya shilingi milioni 435.2 ,  pikipiki 8 na bajaji 2 kwa vikundi hivyo iliyofanyika katika ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya mji wa Bunda.

Sauti ya Katibu tawala wilaya ya Bunda Salmu Alfan Mtelela akiwaasa wanavikundi kutumia fedha za mkopo zinazotolewa na halmashauri kwa lengo lilokusudiwa.

Kwa upande wao wenyeviti wa vikundi hivyo wamesema mikopo hiyo isiyokuwa na riba itawasaidia kujikwamua kimaisha na kuishukuru serikali kwa kutoka mikopo hiyo ya asilimia kumi ya mapato ya ndani ya halmashauri.

Sauti ya wenyeviti wa vikundi wakieezea jinsi mikopo hiyo isiyokuwa na riba itakavyo wasaaidia na kuishukuru serikali.

Vikundi vya akina Mama wakicheza mziki ikiwa ni sehemu ya burani kwenye hafla ya kukabidhi mikopo kwa akina Mama, Vijana na wenye ulemavu. Picha na Amos Marwa

Mikopo hiyo ya asilimia 10 ambayo inatolewa na Serikali ni sehemu ya kuimarisha maendeleo kwa jamii na kuepusha makundi hayo kuingia katika mikopo yenye riba kubwa.

Katibu tawala wilaya ya Bunda Salmu Alfan Mtelela akizindua pikipiki 8 zilizo kabidhiwa kwa vikundi vya vijana ikiwa ni sehemu ya mkopo huo. Picha na Amos Marwa