Bunda FM Radio

Mwenyekiti bodi ya maji Bunda akagua mradi wa maji Mgango-Kiabakari

June 20, 2025, 6:12 pm

Mwenyekiti wa Bodi ya Maji Joshua Mirumbe alievaa suti akitoa maelekezo ya utekelezaji wa mradi wa Mgango-Kiabakari kwa viongozi wa wakala wa maji na usafi wa mazingira Bunda (BUWASSA). Picha na Amos Marwa

Vijiji vyote vilivyopitiwa na mradi wa maji ikiwemo Bisarye, Nyamswa,Ikizu na Bukama vinufaike na mradi ili kupunguza uharibifu kwa miundombinu ya maji kwa vijiji ambavyo sio wanufaika” Joshua Mirumbe Mwenyekiti wa Bodi ya Maji Wilaya ya Bunda

Na Amos Marwa

Mwenyekiti wa  Bodi ya maji wilaya ya Bunda Joshua Mirumbe amewataka wakala wa Maji na usafi wa mazingira (BUWASSA)kuongeza kasi ya utekelezaji wa Mradi wa Maji wa  Mgango-Kiabakari ili wananchi waweze kupata huduma ya maji kwa wakati.

Mirumbe ameyasema hayo alipokagua mradio huo wenye thamani ya bilioni 80.3 na kusema kuwa wananchi wanahitaji maji  kwa haraka na kuongeza kuwa vijiji vilivyopitiwa na mradi watanufaika na maji ikiwemo Bisarye, Nyamswa na Ikizu.

Sauti ya Mwenyekiti wa Bodi ya Maji wilaya ya Bunda Joshua Mirumbe akiwataka Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Bunda (BUWASSA) kuongeza kasi ya utekelezaji wa Mradi wa Mgango-Kiabakari.

 Kaimu Mkurugenzi wa Wakala wa maji safi na usafi wa mazingira Bunda (BUWASSA), Daudi Ashraf akielezea hatua ya utekelezaji wa mradi wa maji wa Mgango-Kiabakari. Picha na Amos Marwa

Nae, kaimu Mkurugenzi wa Wakala wa maji safi na usafi wa mazingira (BUWASSA), Daudi Ashraf amesema kuwa mradi huo umeanza  Februari  mwaka huu na umetekelezwa kwa asilimia 15 na unatarajiwa kukamilika  mwezi januari ,2026.

Sauti ya kaimu Mkurugenzi wa Wakala wa Maji safi na usafi wa mazingira Bunda (BUWASSA), Daudi Ashraf akielezea kuwa mradi utatumia muda wa mwaka mmoja mpaka kukamilika.
Sehemu ya Mtaro uliopo Bisarye uliochimbwa na kampuni ya mkandarasi ya Mori and Gati kwa ajili ya kuweka mabomba yakayosafirisha maji. Picha na Amos Marwa

Wananchi wa kata ya Nyamswa ambapo mradi huo umepita wamesema kukamilika kwa mradi kutawasaidia kuondokana na adha ya Maji ambayo imekuwa kilio chao cha muda mrefu.

Sauti za Wananchi wa kata ya Nyamswa ambapo mradi huo umepita wakielezea watakavyo ondokana na adha ya maji pindi mradio huo utakapo kamilika.

Mradi huo wa  Mgango-Kiabakari Utagharimu jumla ya bilioni 80.3 mpaka kukamilika huku ukitarajia kunufaisha zaidi ya wananchi 51,000.

Tenki lilojengwa Butiama lenye ujazo wa lita milioni 2.5 litakalotumika kusambaza maji kwa wananchi kutoka kwenye mradi huo. Picha na Amos Marwa