Bunda FM Radio

Wananchi Bunda kuchagua viongozi waadilifu, waleta maendeleo

May 21, 2025, 11:20 am

Kibao kinachowakaribisha wageni wanapoingia wilayani Bunda. Picha na Amos Marwa

”Siasa ni maisha lazima tuchague viongozi wanaokuwa karibu na wananchi na wanaojuwa maisha ya wananchi wanaowaongoza”, maoni ya mwananchi wilayani Bunda.

Na Amos Marwa

Wananchi Wilayani Bunda wamesema kueelekea Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Octoba mwaka huu wamejipanga kuchagua Viongozi waadilifu, wasio kula Rushwa na wanaojuwa changamato zao.
Wakizungumza na BUNDA FM, Wananchi hao wamesema  kumekuwa na Tabia ya baadhi ya Viongoziamabao sio waadilifu, hawapo karibu na Wananchi katika kutatua kero zao na kuahidi kuwa uchaguzi wa mwaka huu watachagua Viongozi waadilifu na wenye kuwaletea maendeleo.

Sauti za wananchi wakitoa maoni yao kuhusu aina ya viongozi watakaowachagua

Uchaguzi mkuu unatarajiwa kufanyika Octoba 25, 2025 kotenchini ili kupata Madiwani, Wabunge na Rais watakao kuwa madarakani kwa miaka mitano ijayo kwa mujbu wa katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Baadhi ya wananchi katika kituo kipya cha mabasi wilayani Bunda ambao wametoa maoni yao kuhusu viongozi wanaotarajia kuwachagua katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwezi wa kumi 2025. Picha na Amos Marwa.