Bunda FM Radio

Zaidi ya shilingi milioni 900 kukarabati soko la Manjebe Bunda

April 23, 2025, 2:49 pm

Bidhaa mbalimbali za wafanyabiara katika soko la Manjebe. Picha na Amos Marwa

Wafanyabiashara wengi wilayani Bunda kupata fursa ya kuongeza vipato vyao kwa kuongezwa ukubwa wa soko

Na Adolf Mwolo

Zaidi ya shilingi milioni 900 zinatarajiwa kutumika kukarabati soko la Manjebe lililoko kata ya Nyasura wilaya ya Bunda mkoani Mara.

Akizungumza na Bunda fm Radio Diwani wa kata hiyo Samweli Kiboko amesema kuboreshwa kwa soko hilo kutaongeza kipato katika kata hiyo na kwa wafanya biashara wa bidhaa za jumla wa mkoa wa Mara na jamii kwa ujumla.

Diwani wa kata ya Nyasura akiongea juu ya ujenzi wa soko la Manjebe