Bunda FM Radio

Wakulima nchini watakiwa kupima afya ya udongo

April 23, 2025, 10:28 am

Wakulima wakifurahi baada ya kupata elimu juu ya upimaji wa afya ya udongo Picha Revocutus Andrew

Wakulima wameshauriwa kuwa na utaratibu wa kupima afya ya udongo kabla msimu wa kilimo kuanza

Na.Revocutus Andrew

Wakulima nchini wametakiwa kupima afya ya udongo pamoja na kulima  kilimo asilia.

Hayo yamezungumzwa Leo  na  Bensoni Mturi afisa Teknolonjia za kilimo kutoka Halmashauri ya wilaya ya Bunda  katika  kikao Cha jukwaa la wadau wa kilimo “Development support organization (BUFADESO), kilichofanyika katika ukumbi wa Harieth uliopo katika Halmashauri ya  wilaya ya Bunda mjini na kuwataka  wakulima wote nchini  kujenga tabia ya  kupima udongo kabla ya kupanda mbegu za mazao  Yao ili  kuongeza ufanisi wa uzalishaji shambani na kukuza kilimo na vipato vya wakulima.

 Mturi amesema wakulima wahakikishe  wanatumia kilimo asilia na  ikiwemo matumizi ya mbegu za  asili, mbolea na dawa ili kuachana na mazoea ya kutumia dawa za kemikali kuua wadudu na mbolea za kisasa  badala yake watumie dawa za asili Ili  kuepukana na madhara yatokanayo na dawa za kisasa.

Mwenyekiti Wa Wakulima akizungumza mara baada ya zoezi la upimaji wa afya ya
udongo