Kabanga yawatunuku vyeti vya utumishi bora wafanya kazi
Buha FM Radio

Kabanga yawatunuku vyeti vya utumishi bora wafanya kazi

December 21, 2025, 7:25 pm

Mganga mfawidhi wa hospitali ya rufaa Kabanga Dakitari bingwa wa upasuaji Ndg. Peter Kitenyi wakati kukabidhi vyeti vya utumishi bora wa mwaka 2025. Picha na Sharifat Shinji.

Watumishi wa hospitali ya rufaa Kabanga wamekutana kwa pamoja kusherehekea shelehe ya funga mwaka ilizoambatana na burudani mbalimbali na utunukiwaji wa vyeti kwa baadhi ya watumishi waliofanya vizuri katika idara zao kwa mwaka 20225.

Na; Sharifat Shinji

Hospitali ya rufaa Kabanga imewapongeza na kuwatunuku vyeti vya utumishi bora baadhi ya wafanya kazi wa hospitali hiyo iliyopo Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma lengo likiwa kuongeza hamasa ya utendaji kazi wa watumishi hao.

Pongezi hizo zimetolewa na Mganga mfawidhi wa hospitali hiyo Dakitari bingwa wa upasuaji Ndg. Peter Kitenyi wakati wa hafla ya kufunga mwaka 2025 iliyofanyika Jumamosi ya Desemba 20 katika ukumbi wa Bwami Dubai katika Halmashauri ya Mji Kasulu na kusema umekuwa mwaka wa mafanikio licha ya changamoto mbalimbali zilizojitokeza.

“Ndugu zangu kwanza tujipongeze mwaka umeisha salama tumefanya kazi kubwa sana licha ya changamoto za hapa na pale lakini Kabanga imebaki salama hivyo tuendelee kufanya kazi kwa ushirikiano”Amesema Dkt. Kitenyi.

Watumishi wa hospitali ya rufaa Kabanga wakiwa katika ukumbi wa Bwami Dubai kwa ajili ya hafla ya funga mwaka 2025. Picha na Sharifat Shinji.

Aidha Dkt. Katenyi amesema hospitali ya Kabanga inatarajia kuanza ujenzi wa Maabara kubwa ya kisasa ili kuboresha utoaji wa huduma kwa wagonjwa na wanafunzi wanaofika pale kwa ajili ya kujifunza kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi.

“Leo kuna baadhi mmepata vyeti vya watumishi bora wa mwaka 2025 lakini tunatarajia kuanza ujenzi wa Maabara kubwa ya kisasa kwa ajili ya kuongeza ubora wa utendaji kazi na kutoa huduma bora kwa wagonjwa na wale wote wanaokuja kujifunza hospitalini kwetu” Amesema Dkt. Kitenyi.

Dkt. Katenyi akizungumza katika hafla ya watumishi wa hospitali ya rufaa Kabanga. Picha na Sharifat Shinji.

Katika hatua nyingine Dkt. Kitenyi amemalizia kwa kusema Askofu Joseph Roman Mlola,ambaye ni Askofu wa jimbo katoriki Kigoma, pia mlezi na mmiliki wa wa hospitali hiyo anatambua uwepo wa watumishi hao kwa kuambatanisha ujumbe wa salamu za pongezi.

“Muda mfupi nimezungumza na Baba Askofu anatambua uwepo wenu hivyo anawasalimia na ametuma ujumbe wa pongezi kutoka jimboni kwa hiyo endeleeni kupongezana kwa kumshuru Mungu kwa kumaliza mwaka tukiwa wazima wa afya”Amesema Dkt. Kitenyi.

Dkt. Katenyi akiwa katika meza kuu akizungumza na watumishi wa hospitali hiyo. Picha na Sharifat Shinji.

Hospitali ya Kabanga iliyo chini ya kanisa Katoliki jimbo la Kigoma  ilipata usajili kwa mara ya kwanza kama hospitali binafsi mwaka 1997 na kupewa hadhi ya kuwa hospitali ya rufaa mwaka 2010 chini ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa huduma kwa wananchi zaidi ya million 2.3 wa Mkoa wa kigoma na maeneo mengine nchini.