CRDB kuwanufaisha wakulima wa mazao ya chakula wilayani Buhihigwe
Buha FM Radio

CRDB kuwanufaisha wakulima Buhigwe

December 13, 2025, 3:25 pm

Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya CRDB kuhusu mikopo ya wakulima wa Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe. Picha na Sharifat Shinji.

Wakulima wilayani Buhigwe kupitia kwa mbunge wa jimbo la Buhigwe Prof. Pius Yanda wamenufaika na mafunzo ya mikopo kutoka Taasisi ya kifedha ya Bank ya CRDB kwa ajili ya kuendesha shughuli za kilimo kupitia mikopo hiyo.

Na; Sharifat Shinji

Wakulima katika Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe wamehudhuria semina ya mafunzo ya kilimo iliyoandaliwa na Bank ya kibiashara CRDB kwa lengo la kujifunza maswala ya mikopo kwa ajili ya kilimo cha mazao ya chakula katika Halmashauri hiyo.

Wakizungumza na Buha FM Radio baadhi ya wakulima waliohudhulia semina hiyo wamesema elimu walioipata itaenda kuwasaidia hasa katika maswala ya mikopo na kuiomba serikali iwasaidie kukidhi vigezo vya kupata mikopo hiyo ili waweze kunufaika nayo.

Sauti za wakulima wilayani Buhigwe.

Aidha kwa upande wake muwezeshaji wa mafunzo hayo  Peter Christopher Meneja wa CRDB makao makuu na msimamizi wa mradi wa kilimo cha mazao lishe amesema malengo ya kuwafikia wakulima wa mazao ya chakula wa Halmashauri hiyo ni kuongeza usalama wa chakula na kuwezesha uhimilivu wa mabadiliko ya tabia ya nchi.

Sauti ya muwezeshaji wa mafunzo hayo  Peter Christopher Meneja wa CRDB makao makuu.
Katika ni muwezeshaji wa mafunzo hayo  Peter Christopher Meneja wa CRDB makao makuu na msimamizi wa mradi wa kilimo cha lishe akiwa na viongozi wengine wa Wilaya Buhigwe. Picha na Sharifat Shinji.

Muwezeshaji huyo ameongeza  kwa kusema mradi huo umelenga kuwafikiwa wanufaika zaidi ya milioni 6 wa moja kwa moja na wasio wa moja kwa moja ndani ya kipindi cha miaka 20 ya utekelezaji wa mradi huo huku wakiwa wamewafikia zaidi ya wanufaika laki tano na kutoa pesa zaidi ya bilioni 100 kwa wanufaika hao.

Sauti ya muwezeshaji wa mafunzo hayo  Peter Christopher Meneja wa CRDB makao makuu.

Katika hatua nyingine Kaimu Mkurugenzi katika Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe Hamza Mnaliwa amesema ili wakulima wapige hatua katika shughuli zao za kilimo ni lazima kupata mikopo midogo midogo ili kuwasaidia kuendesha  kazi zao za kilimo huku akiwataka wakulima kuzingatia uaminifu wa kurejesha mikopo hiyo kwa wakati.

Kaimu Mkurugenzi katika Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe Hamza Mnaliwa.
Kaimu Mkurugenzi katika Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe Hamza Mnaliwa akingungumza mbele ya washiriki wa mafunzo ya CRDB. Picha na Sharifat Shinji.

Mafunzo hayo yameandaliwa na Mbuhge wa Jimbo la Buhigwe na yamewaleta pamoja maafisa wa CRDB kwa ajili ya kutoa elimu ya mikopo kwa  wakulima wa Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe, Madiwani, watendaji wa kata na maafisa ugani kutoka kata zote za Halamashauri hiyo kwa lengo la kuwasaidia wananchi wa Buhigwe kupata mikopo katika shughuli za kilimo.