Buha FM Radio

Bodaboda Kigoma wagomea maandamano ya Desemba 9

December 7, 2025, 12:20 pm

Baadhi ya maafisa usafirishaji kutoka Wilaya mbalimbali katika Mkoa wa Kigoma wakiwa katika mkutano wa pamoja wilayani Kasulu. Picha na Sharifat Shinji.

Maafisa usafirishaji maalufu Bodaboda kutoka Wilaya mbalimbali mkoani Kigoma wapinga maandamano yaliyopangwa kufanyika Desemba 9, Serikali wilayani Kasulu yatia neno la msisistizo wa kutojihusisha na maandamano hayo.

Na; Sharifat Shinji

Maafisa Usafirishaji wa abiri malufu Bodaboda mkoani Kigoma wamesema hawatoshiriki Maadamano yaliyopangwa kufanyika Desemba 9 mwaka huu na kusema watakuwa mabalozi wa kuzuia vitendo vya uvunjifu wa amani katika Mkoa wa Kigoma na taifa kwa ujumla.

Wakizungumumza katika kikao cha pamoja na cha Maafiasa hao kutoka Wilaya mbalimbali za Mkoa wa Kigoma kilichofanyika katika Halmashauri ya Mji Kasulu akiwemo Makamo Mwenyeiti wilaya ya Kasulu Hamad Kilugu na Mwenyekiti bodaboda Wilaya ya Buhighwe Zaeli Livingstone wamesema  watahimiza amani na kutojihusisha na maandamano ya Desemba 9.

Sauti ya viongozi wa bodaboda Wilaya ya Kasulu na Buhigwe.

Aidha Jeff Mkando ambaye ni Afisa habari wa bodaboda na  bajaji mkoa wa Kigoma amepiga marufuku kwa maafisa wote mkoani humo na kuelekeza viongozi kuanzia ngazi za kata hadi Mkoa wanasimamia zoezi la kutoshiriki maandamano hayo.

Sauti ya Jeff Mkando Afisa habari wa bodaboda na  bajaji mkoa wa Kigoma.

Kwa upande wake mwakilishi wa mgeni rasmi wa mkutano huo Adriano Mihale Afisa Mtendaji Kata ya Asante Nyerere na Kaimu Afisa Tarafa Heruchini ambaye alikuwa akimwakilisha Mkuu wa Wilaya Mhe. Kanal Isack Mwakisu, amesema ofisi ya mkuu wa Wilaya imesisiti vitendo vya vurugu za maandamano wasijihusishe kwa namna yoyote kwani vitendo hivyo vina madhara makubwa kama yaliyotokea Oktoba 29 mwaka huu.

Sauti ya Afisa Mtendaji Kata ya Asante Nyerere na Kaimu Afisa Tarafa Heruchini Bw. Adriano Mihale akimwakilisha Mkuu wa Wilaya Mhe. Kanal Isack Mwakisu.
Afisa Mtendaji Kata ya Asante Nyerere na Kaimu Afisa Tarafa Heruchini Bw. Adriano Mihale akimwakilisha Mkuu wa Wilaya Mhe. Kanal Isack Mwakisu. Picha na Sharifat Shinji.

Kikao hicho kilikuwa na ajenda mbalimbali ikiwemo kuwasilisha changamoto  zinazowakabili hasa kuelekea mwisho wa mwaka ambapo huwa wanakutana na usumbufu wa  vyombo vya usalama ambapo wameiomba serikali  kuzipatia ufumbuzi changamoto hizo.