Buha FM Radio

Waapa kukusanya mapato na kusimamia miradi ya maendeleo

December 3, 2025, 5:07 pm

Madiwani wa Halmashauri ya Mji Kasulu wakitia sahii viapo vya kuwatumikia wananchi wa kata zao. Pisha na Sharifat Shinji.

Madiwani wa Kata mbalimbali katika Halmashauri ya Mji Kasulu wameahidi kusimamia miradi yote ya maendeleo pamoja na kusimamia ukasanyaji wa mapato katika Halmashauri hiyo ili kuiwezesha serikali kujitegemea kupitia mapato ya ndani.

Na; Sharifat Shinji

Madiwani wateule katika Halmashauri ya Mji Kasulu mkoani Kigoma amekula kiapo cha kuwatumikia wananchi wa halmashauri hiyo huku wakiahidi kusimamia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ukusanyaji wa mapato katika kata zao.

Zoezi hilo la uapisho limefanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji Kasulu mbele ya Hakimu mkaazi mwandamizi wa mahakama ya Wilaya, Iman David Matenzi, ambapo baadhi ya Madiwani hao akiwemo Elisha Bakena Diwani wa kata ya Mrusi, ameahidi kusimamia miradi ya maendeleo kwa uadilifu, kuwasimamia wananchi kikamilifu pamoja na kutatua migogoro ya wananchi katika Kata zao.

Sauti ya Elisha Bakena Diwani wa kata ya Mrusi.

Awali akitoa salamu kutoka mkoani Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Ndg. Elisante Mbwilo amewataka Madiwani kwenda kuwatumikia wananchi bila upendeleo pamoja na  kusimamia ukusanyaji wa mapato kama ilivyoagizwa na Rais kuwezesha serikali kujitegemea kiuchumi na kuwezesha Halmashauri kuongeza mapato na kumudu gharama uendeshaji wa Miradi yake.

Sauti ya Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Ndg. Elisante Mbwilo.
Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Ndg. Elisante Mbwilo akitoa salamu kutoka ofsi ya Mkoa. Picha na Sharifat Shinji.

Aidha amewataka madiwani hao kushirikiana kwa miaka yote mitano ili kuleta usawa, uwazi, uadilifu na utawala wa sheria ili kuleta matumizi bora ya rasilimali katika Halmashauri hiyo kwa misingi ya maendeleo endelefu.

Sauti ya Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Ndg. Elisante Mbwilo.

Katika hatua nyingine Evelin John ambaye ni Diwani wa viti malumu kutoka kata ya Heru Juu amesema ataenda  kusukuma usimamizi wa masoko yote ya kimkakati wanayasimamia kimamilifu ili kuleta mapato katika Halmashauri pamoja na kuanzisha vikundi vya watu wa jinsia zote ili wananchi wanufaike na miradi mikopo ya Halmashauri.

Sauti ya Evelin John ambaye ni Diwani wa viti malumu kutoka kata ya Heru Juu.
Baadhi ya Madiwani wakiwa katika ukumbi wa Halmashauri baada kula kiapo cha kuwatumikia wananchi wa Halmashauri ya Mji Kasulu.Picha na Sharifat Shinji.

Hata hivyo madiwani hao wamemchagua kwa kumpigia kura Ayubu Ngalaba kuwa mwenyekiti wa barazahilo linaloundwa na Madiwani wa kata 15 pamoja na madiwani wa viti maalumu kukamilisha madiwani 20 huku Ndg. Ayubu Mgalaba akiahidi kusimamia kwa uadilifu Baraza hilo.

Ayubu Ngalaba baada ya kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji kasulu kupitia baraza ya Madiwani. Picha na Sharifat Shinji.