Buha FM Radio

World Vision Tanzania yahimiza kutunza miradi ya maendeleo

November 26, 2025, 12:40 am

Baadhi ya viongozi wa World Vision na wadau wa maendeleo katika picha ya pamoja baada ya kikao cha wadau wa maendeleo wilayani Kasulu. Picha na Ramadhan Zaidy.

Wadau wa maendeleo wa miradi ya World VisionTanzania katika Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu wameombwa kuitunza miradi inayotekelezwa na shirika hilo ili ije kusaidia vizazi vijavyo.

Na; Ramadhan Zaidy

Shirika la maendeleo la World Vision Tanzania linalotekeleza miradi katika Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma limewataka Wanufaika wa miradi hiyo kuitunza na kuilinada miradi yote inayojengwa na kuendelezwa mkoani humo ili iweze kunufaika kwa muda mrefu.

Wito huo umetolewa na Meneja wa Western Cluster Jacklin Kaihura wakati wa kikao kilichowakutanisha wadau wa miradi inayosimamiwa na kuendeshwa na Shirika hilo, wilayani humo na kusema kutunzwa na kuendelezwa kwa miradi hiyo kutasaidia wananchi wengi na kunufaika kizazi cha badae.

Sauti ya Meneja wa Western Cluster Jacklin Kaihura wakati wa kikao kilichowakutanisha wadau wa miradi World Vision Tanzania.
Baadhi ya  wananchi na wanufaika wa miradi ya World Vision Tanzania.Picha na Ramadhan Zaidy.

Kwa upande wake Mratibu wa Miradi ya Buhoro na Nyakitoto Esther Mshendwa ameeleza shughuli zilizotekelezwa na shirika hilo na ikiwa ni pamoja na Afya na lishe, maji na   Utunzaji wa mazingira, elimu, jinsia ulinzi na haki za mtoto katika jamii.

Sauti ya Mratibu wa Mradi ya Buhoma na Nyakitoto Esther Mshendwa.

Aidha Mratibu Bi. Mshendwa ameongeza kuwa shirika hilo limetoa mafunzo kwa wazazi juu ya ulinzi wa mtoto na mwanamke pamoja na kutoa mikopo kwa ajili ya kujiinua kiuchumi kwa wanufaika wa mradi huo.

auti ya Mratibu wa Mradi ya Buhoma na Nyakitoto Esther Mshendwa.

Naye Mgeni rasmi katika Kikao hicho ambaye ni Mkurungenzi wa Halmashari ya Wilaya ya Kasulu, Francis Kafuku amelipongeza shirika la world Vision kwa kuendeleza miradi mbalimbali wilayani Kasulu na kuboresha maisha ya wananchi.

Sauti ya Mkurungenzi Mkurugenzi wa Halmashari ya Wilaya ya Kasulu Francis Kafuku.

Katika hatua nyingine baadhi ya  wananchi na wanufaika wa miradi hiyo wamesema katika kipindi chote cha utekelazi wa miradi, shirika hilo limewasaidi kujiinua kiuchumi pamoja na kupata elimu za ujasiliamali.

Sauti za baadhi ya  wananchi na wanufaika wa miradi ya World Vision Tanzania.

Shirika la World Vision Tanzania ni shirika la kikisriso lisilo la kiserikali lenye kufanya shughuli mbalimbali ndani na nje ya nchi likiwa limejikita katika kuinua jamii katika sekta mbalimbali ili kufanya istawi kwa kulenga zaidi watoto, Wakiwemo watoto wanaishi mazingira magumu.