Buha FM Radio

Dini mbalimbali Kasulu zabariki uchaguzi mkuu 2025

September 10, 2025, 10:04 pm

Waumini wa dini mbalimbali wakiwa katika ukumbi wa Chuo cha walimu Kasulu TTC wakifuatilia ibaada iliyokuwa ikitolewa katika kongamano la kuombea uchaguzi mkuu 2025. Picha na Sharifat Shinji.

“Watanzania angaliyeni mataifa mengine nilipata nafasi ya kwenda Sudan kwenye ukaguzi unaona namna wananchi wanavyohangaika hadi watoto wadogo wanajuwa namna ya kuomba msaada pia nilienda Congo na kwenyewe niliona namna watu wanavyoteseka kuitafta amani nikawa nawaza Watanzania wangekuwa wanapata nafasi ya kutoka wangejifunza namna Amani ilivyo na umhimu katika jamii” Amesema IGP. Siro.

Na; Sharifat Shinji

Kuelekea uchaguzi mkuu utakaofanyika Octoba 29, 2025 waumini wa Dini mbalimbali katika Halmashauri ya Mji Kasulu Mkoani Kigoma wamekusanyika na kuandaa kongamano la ibaada ya kuombea uchaguzi mkuu pamoja na kuwaombea wagombea katika nafasi mbalimbali za uongozi nchini.

Kongamano hilo la ibada limefanyika katika Ukumbi wa Bwalo la Chuo cha Walimu Kasulu TTC Septemba 09 na kuhudhuliwa na mgeni rasimi ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Kigoma IGP Mstafu, Mhe. Balozi Saimon Siro pamoja na Wakurugenzi wa Wilaya ya Kasulu na Viongozi mbalimbali wa dini.

Sheikh Nasibu Rajabu ambaye ni Sheikh wa Mkoa Shia (TIC) ameeleza namna amani ambavyo inaweza kuwaweka pamoja Watanzania huku akihubiri maneno ya Mtume Mohammad (S.A. W) juu amani kwa wananchi.

Sauti ya Sheikh wa Mkoa Shia akieleza na kuhubili amani
Sheikh wa Mkoa Shia Nasibu Rajabu akihutubia waumini wa dini mbalimbali katika kongamano la kuombea uchaguzi mkuu 2025 katika Wilaya ya Kasulu. Picha na Sharifat Shinji.

Kupitia kongamano hilo IGP Siro ambaye ni mgeni rasmi amesema ili Taifa liendelee kuwa salama ni lazima viongozi wa dini washikamane kwa kuliombea Taifa na kulinda amani iliyopo katika Taifa la Tanzania na kusisitiza umuhimu wa viongozo wa dini katika Jamii.

Sauti ya IGP Saimon Siro akizungumza na waumini wa dini mbalimbali katika kongamano la kuombea uchaguzi mkuu mwaka huu.
IGP Mstafu, Balozi Saimon Siro akizungumza katika Kongamano la dini mbalimbali wilayani Kasulu.

Aidha IGP ameongeza kwa kuwaomba viongozi wa dini kuhubiri dini kwa kuzingatia mipaka yake pamoja na kuzingatia maadili ya Watanzani ambayo yataendelea kudumisha amani katika Taifa la Tanzania huku akiwataka wazazi kuhusika katika maelezi ya watoto  katika familia ili kutengeneza jamii iliyo bora.

Sauti ya IGP Saimon Siro akizungumza na waumini wa dini mbalimbali katika kongamano la kuombea uchaguzi mkuu mwaka huu.
Waumini wa dini mbalimbali wakiwa katika kongamano la pamoja la kuombea uchaguzi mkuu mwaka 2025. Picha na Sharifat Shinji.

Katika hatua nyingine Kamanda Siro amesema katika swala la uchaguzi serikali imejipanga kusimamia kikamilifu huku akiwasisitiza wananchi kusikiliza kampeni za wagombea na kuwaomba kushiriki siku ya kupiga kura huku akitaja maendeleo yaliyofanyika katika Mkoa wa kigoma chini ya Dkt. Samia Suluhu Suluhu Hassan.

Sauti ya IGP Saimon Siro akizungumza na waumini wa dini mbalimbali katika kongamano la kuombea uchaguzi mkuu mwaka huu.
Mgeni rasmi wa kongamano mkuu wa Mkoa wa Kigoma IGP Siro katikati kulia ni Askofu Josephat Kilibaze mwenyekiti wa kamati ya maridhiano Tanzania kushoto mkuu wa Wilaya ya Kasulu Kanal Isack Mwakisu. Picha na Sharifat Shinji.

Akimalizia Askofu Josephat Kilibaze Mwenyekiti wa Kamati Maridhiano Tanzania amewakumbusha viongozi wa dini kuhakikisha wanayachukuwa yote yaliyosemwa na Mgeni rasmi juu ya mipaka na kuyazingatia yote waliyoyahubiri kwenye Kongamano hilo ili kulinda amani kuelekea uchaguzi mkuu mwaka huu.

Sauti ya Askofu Josephat Kilibaze akihutubia katika kongamano la kuombea uchaguzi mkuu 2025.

Kongamano hilo limefanyika mahususi kwa ajili ya kuombea uchaguzi mkuu mwaka 2025 utakaofanyika Octoba 29 pamoja na kuwaombea nafasi ya Udiwani, Ubunge na Urais katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Taifa kwa ujumula ili kudumisha amani ya Watanzania.

Waumini wa dini mbalimbali wakiwa katika ukumbi wa Chuo cha walimu Kasulu TTC wakifuatilia ibaada iliyokuwa ikitolewa katika kongamano la kuombea uchaguzi mkuu 2025. Picha na Sharifat Shinji.