Buha FM Radio

Dkt. Samia kutua Kasulu Septemba 13

September 8, 2025, 1:01 pm

Msafara wa Mkuu wa Wilaya ya Kasulu kwenye Mbio za Polepole (Jogging) zilizofanyika kwa ajili ya Bonanza la kuukaribisha Mwenge wa Uhuru 2025. Picha na Sharifat Shinji.

Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Mhe. Kanal Isack Mwakisu amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM atafanya kampeni katika Wilaya ya Kasulu Septemba 13 mwaka huu.

Na; Sharifat Shinji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mgombea Urais kupitia cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwasili wilayani Kasulu mnamo Septemba 13 mwaka huu kwa ajili ya kunadi sera zake za kampeni za uchaguzi mkuu utakaofanyika Octoba 29 mwaka huu.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Mhe. Kanal Isack Mwakizu wakati wa ufunguzi wa Bonanza la kuukaribisha mwenge wa Uhuru mwaka 2025 lililofanyika October 6 katika uwanja wa Kiganamo katika halmashauri ya Mji Kasulu.

Sauti ya Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Mhe. Mwakisu akitoa taarifa ya ujio wa Rais Samia katika Wilaya ya Kasulu.
Mkuu wa Wilaya Katikati, kulia ni Mwenyekiti wa Chama Chamapinduzi Wilaya ya Kasulu Mbelwa Abdalla Kushoto ni Mudau wa Bonanza lililofanyika uwanja wa Kiganamo Halmashauri ya Mji Kasulu wakifuatilia Michezo mbalimbali katika uwanja huo. Picha ya Sharifat Shinji

Aidha Mwakisu  amewasisitiza wananchi kushiriki kampeni kwa amani na utulivu pamoja na kujitokeza kushiriki uchaguzi mkuu kwa amani na utulivu siku ya tarehe 29 mwezi octoba mwaka huu.

Sauti ya Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Mhe. Mwakisu akiwaomba wananchi kujitokeza kusiriki uchaguzi mkuu Octoba 29 mwaka huu.

Katika hatua nyingine akizungumza Rebeka Eza ambaye ni Afisa Mipango Halmashauri ya Mji Kasulu ambaye ni mdau wa bonanza amewasisitiza wananchi wa Wilaya Kasulu kujitokeza kushiriki uchaguzi mkuu wa Octoba 29 mwaka huu.

Sauti ya Afisa Mipango Halamashauri ya Mji Kasulu akizungumzia umhimu wa uchaguzi mkuu.

Hata hivyo Bonanza hilo limeandaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kasulu kwa ajili ya mapokezi ya mbio za mwenge wa Uhuru mwaka 2025 likiwa na kauli mbio isemayo “jitokeze kushiriki uchaguzi mkuu mwaka 2025 kwa amani na Utulivu”.