Buha FM Radio

Wawili wafariki Kasulu chanzo kuhara na kutapika

August 27, 2025, 9:19 pm

Mratibu wa Afya kwa Umma Ndg. Mwita Range. Picha na Sharifat Shinji 

Kwa mama mwenye mtoto anatakiwa baada ya kumsafisha mtoto kuhakikisha ananawa  mikono vizuri kumkinga mtoto,  hata hivyo viongozi wa taasisi, masoko wanatakiwa kuweka maji tiririka  amesema  mratibu Mwita.

Na Irene Charles

Wananchi Kasulu watakiwa kuchukua taadhari  ili kuepukana na tatizo la kuhara na kutapika kwa kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni , matumizi sahihi ya choo kwa kuwa safi mda wote, kuepuka kusalimiana au kupongezana kwa njia ya mkono.

Afisa Afya wa Halmashauri ya Mji Kasulu Ndg. Malimi Temi. Picha na Sharifat Shinji 

Hayo yamebainishwa na  afisa afya wa halmashauri ya Mji Kasulu Ndg. Malimi Temi  kupitia kipindi cha shangwe la asubuhi amesema mwananchi atakaebaini dalili za kuhara na kutapika anatakiwa kufika kituo cha afya ili kupata huduma mapema.

Sauti ya Ndg. Malimi Temi Afisa Afya wa Halmashauri ya Mji Kasulu.

Afisa Malimi amesema kwa sasa wamepata dawa ya vidonge kwaajili ya kutibu maji kwa gazi ya kaya, wahudumu ngazi ya jamii watapita kutoa dawa hiyo kwa wananchi ambao wamepatwa na changamoto hiyo huku wakiendelea kuangalia vyanzo vya maji.

Sauti ya Ndg. Malimi Temi Afisa Afya wa Halmashauri ya Mji Kasulu.

Kwa upande wake mratibu wa afya kwa umma Ndg. Mwita Range  amesema usafi  sehemu ya kuandalia chakula  pamoja na vyombo  unaitajika kwa kiwago cha juu  na  kulinda maji na vyanzo vyake  ili kuepusha kupata  vimelea.

Sauti ya Mratibu wa Afya kwa Umma Ndg. Mwita Range.

Kwa mama mwenye mtoto anatakiwa baada ya kumsafisha mtoto kuhakikisha ananawa  mikono vizuri kumkinga mtoto,  hata hivyo viongozi wa taasisi, masoko wanatakiwa kuweka maji tiririka  amesema  mratibu Mwita.

Sauti ya Mratibu wa Afya kwa Umma Ndg. Mwita Range.
Afisa Lishe Ndg. John Sabatele. Picha na Sharifat Shinji.

Aidha afisa lishe Ndg. John Sabatele  amesema kuhara na kutapika kunaweza kusababisha upungufu wa  lishe mwilini   kwa  kukosa virutubisho na kupata utapiamlo , muda mwingine kupelekea mpaka kifo.

Sauti ya Afisa Lishe Ndg. John Sabatele.

Mpaka sasa watu wawili wamepoteza maisha kutokana na ungonjwa huu ambao haujajulikana mmoja akitoka  kata ya Kigondo mtaa wa Nyarumanga na wapili   kutoka kata ya Murusi mtaa wa Hwazi