Buha FM Radio

Viongozi wa serikali za mitaa Kasulu waapishwa

April 23, 2025, 1:54 pm

Viongozi wa serikali za mitaa wakila kiapo. picha na Ramadhani Zaidy.

Mkurugenzi mtendaji katika wilaya ya Kasulu Vijijini amewapongeza viongozi hao kwa nafasi waliyochaguliwa.

Na Sungura Jeremiah

Viongozi wa Teule wa Serikali za mitaa katika Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu wamejitokeza katika zoezi la uapisho uliofanyikia katika ukumbi wa wa Bogwe Sekondari katika Halmashauri ya Mji Kasulu chini ya huku wakiombwa kufata misingi ya kiuongozi.

Uapisho huo umefanyika Novemba  29  chini ya hakimu Mwandamizi Rajabu Fakihikutoka mahakama ya Mwanzo Kasulu Mjini kabla ya Kiapo amewasihi kuendelea kushirikiana na mahaka katika kutatua changamoto za madai kabla ya kufika mahaakamani.

Sauti ya hakimu Mwandamizi Rajabu Fakihi

Aidha Mkurugenzi mtendaji katika wilaya ya Kasulu Dkt. Semistatus Mashimba amewapongeza viongozi hao kwa nafasi waliyochaguliwa huku akiwasihi kufanya kazi na kuacha tofauti za kisiasa bali kuwasaidia wananchi waliopo katika maeneo yao ya kazi.

Sauti ya Dkt. Semistatus Mashimba

Kwa upande wao baadhi ya wiongozi wa kata mbalimbali wameelezea namna watakavyo shirikiana na wananchi kutimiza majukumu yao huku wakitoa wito kwa wananchi kuwapa ushirikiano katika kutekeleza maajukumu yao.

Sauti za viongozi mbalimbali serikali za mitaa

Ifahamike kuwa zoezi la uapisho limefanyika mara baada ya zoezi uchaguzi wa serikali za mitaa ulifanyika Novemba 27 kutamatika na kuwapata viongozi wawakilishi  katika Ngazi ya serikali za mitaa katika kata zote nchini.

Katikati ni hakimu Mwandamizi Rajabu Fakihikutoka mahakama ya Mwanzo Kasulu Mjini, kulia ni Mkurugenzi mtendaji katika wilaya ya Kasulu Dkt. Semistatus Mashimba wakiwa katika ukumbi wa Bogwe sekondari.