Bunda FM Radio

Wanafunzi wote wanapaswa kuripoti shuleni

February 12, 2026, 8:14 pm

Picha ya Katibu tawala Wilaya ya Bunda Salmu Alfan Mtelela akiwaasa madiwani na wananchi wote kupeleke wanafunzi shuleni. Picha na Brown conscious

Tunapaswa kuhakikisha wanafunzi wote wenye sifa wanaenda shule madiwani waote na wakuu wa idara ya elimu mkasimamie hilo na kuzingatia chakula kinapatikana shuleni Kwa ajili ya lishe Kwa wanafunzi” Katibu tawala Wilaya ya Bunda Salmu Alfan Mtelela

Na Amos Marwa

Serikali Wilaya ya Bunda imewataka madiwani Kwa kushirikiana na wananchi wote kuhakikisha wanafunzi ambao hawajaripoti shuleni waweze kuripoti ili Kwendelea na masomo yao.

Hayo yamebainishwa na Katibu tawala Wilaya ya Bunda, Salmu Alfan Mtelela aliemwakilisha mkuu wa Wilaya wakati wa salamu za serikali katika kikao Cha baraza la madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Bunda na kusema kuwa darasa la awali ni Asilimia 92, darasa la kwanza  asimilia 92, na sekondari ni asimilia 94

Sauti ya Katibu tawala Wilaya ya Bunda Salmu Alfan Mtelela akiwaasa madiwani na wananchi wote kupeleke wanafunzi shuleni

Katika hatua nyingine Mtelela amesema wananchi Wilaya ya Bunda wanapaswa kutumia fursa ya bima ya afya Kwa wote  ambayo imetangazwa na serikali kuu ili kupunguza gharama za matibabu Kwa watu wasio na uwezo wa kiuchumi.

Sauti ya Katibu tawala Wilaya ya Bunda Salmu Alfan Mtelela akiwaasa wananchi kutumia fursa ya bima ya afya kwa wote
Picha ya Mkurugenzi wa Mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira Bunda (BUWASSA), Bi. Esther Gilyoma ikiwasilisha utekerezaji wa miradi ya maji katika kikao Cha baraza la madiwani robo ya pili halmashauri ya mji wa Bunda. Picha na Brown conscious

Baraza hilo la madiwani limejadili  na kuazimia masuala mbalimbali ikiwemo Malipo ya fidia ya wananchi walioharibiwa mazoa yao na wanyama , kupokea iaarifa ya utekerezaji wa miradi ya maji kutoka Mamlaka za maji mjini na vijijini, utekerezaji wa miradi ya Barabara , uwekezaji katika mlima Kaswaka  na Ukusanyaji wa mapato Kwa ajili ya maendeleo halmashauri ya mji Bunda.

Baadhi ya Madiwani wa halmashauri ya mji wa Bunda waliohudhuria kikao cha baraza la madiwani robo ya pili februari 12. picha na Amos marwa